Taarifa zilizotufikia muda huu hapa MASSHELE BLOG
 ni kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya imemhukumu miezi mitano jela Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA), Joseph Mbilinyi maarufu kama ‘Sugu’.
Sugu amehukumiwa pamoja na Katibu waCHADEMA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.
  • Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite ambapo amesema ameridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka.