Monday

Hakuna kategoria za virai katika uchanganuzi wa kisintakisia, Kubali au kataa hoja hii kwa kutumia mifano maridhawa

0 comments
Hakuna kategoria za virai katika uchanganuzi wa kisintakisia, kubali au kata hoja hii kwa kutumia mifano maridhawa. Dhana ya kategoria ni pana na imejadiliwa na watalaam mbalimbali ambao wamegawanyika katika pande kuu mbili ambazo ni kundi la wanamapokeo na wanausasa. Neno kategoria ni neno lenye asili ya kigiriki lenye maana ya uarifu(prediction) yaani sifa kuu ya kiima. Wanasarufi mapokeo wanaziona kategoria za kisarufi kuwa ni sifa zinazoambatanishwa kwenye aina za maneno. Kategoria hizo ni kama vile kategoria za nafsi, kategoria za njeo, kategoria ya hali, kategoria ya jenda/jinsia, kategoria ya uhusika na kategoria ya ngeli. Kwa mujibu wa wanausasa wanasema kategoria ni dailojia mbalimbali katika uundaji wa tungo . katika mkabala huu wa kisasa umeonekana kuwa kuna kategoria kuu mbili ambazo ni: I)kategoria ya kileksika(neno) II)kategoria ya virai Kwa mujibu wa swali tutajikita Zaidi katika kuelezea kategoria ya virai. kabla ya kutazama kategoria ya virai ifuatayo ni nmaana ya virai kama ilivyofasiliwa na watalaam mbalimbali: Massamba na wenzake(2009), wanaon kuwa kirai ni kipashio cha kimuundo chenye chenye Zaidi ya neno moja ambacho hakina muundo wa kiima kiarifu. Kihore na wenzake(2007), wanasema kuwa kirai kimefafanuliwa kama kipashio cha kimuundochenye neno moja au Zaidi lakini bila uhusiano wa kiima kiarifu. Kwao mahusiano ya kiima kiarifu ni yale yanayoonyesha anaye tenda jambo na tendo linalotendwa, aneye tenda jambo ni kiima na tendo linalotendwa ni kiarifu. Mfano: mtu mnene/ anachoma nyama. Kiima kiarifu TUKI(2011), kirai ni kipashio chenye Zaidi ya neno moja lakini ambacho hakina muundo wa kiima kiarifu. Fasili zote hizo zina udhaifu. Na udhaifu huo ni kama ifuatavyo: Kusema kuwa kirai kina Zaidi ya neno moja si kweli kwani hata neno moja linaweza kuwa kirai. Mfano: kirai kitenzi kinachoundwa na kitenzi peke yake. Analima ,wanaimba n.k KT T Analima Vile vile kusema kuwa kirai hakina muundo wa kiima kiarifu si sahihi kwani kuna baadhi ya sentensi ambazo zina kiima ambacho hakijidhihirishi waziwazi. Mfano: Anaoga S KN KT N T Q Anaoga Pia dai la kuwa kirai ni tungo isiyokuwa na kitenzi ndan yake si sahihi kwani upo uwezekano wa kirai kuwa na kitenzi ndani yake. Hivyo basi kirai ni kipashio cha kimuundo chenye neno moja au Zaidi chenye neno kuu moja. Kirai kimejikita katika ziadi katika maneno makuu yenye dhima kubwa kisintaksia kama vile nomino, kivumishi, kitenzi, kihusishi, kielezi na kibainishi.hivyo basi aina hizi za maneno yenye dhima kubwa kisintaksia ndio zinatupati aina za virai. Ufuatao ni ushahidi wa kuwepo kwa kategoria za virai: Ushahidi wa kimofolojia: kimofolojia kuna maumbo Fulani yanayothibitisha kuwepo kwa kategoria ya virai nah ii inadhibitika kwa kuangalia viambishi vinavyoambikwa kwenye baadhi ya maneno vikionyesha umoja na wingi. Mfano: baba na mama wanalima Kiti na meza vimevunjika Katika sentensi hizi mbili viambishi vilivyopigiwa msititari vikionyesha umoja na wingi vyenye upatanisho wa kisarufi hudhibitisha kuwepo kwa virai vilivyo katika kategoria moja, kwani vinadhihirisha kuwa vitu vyenye hadhi sawa na visivyo na hadhi sawa haviwezi kusimama pamoja na kuwekewa viambishi hivyo vya umoja na wingi. Ushahidi wa kisemantiki; katika lugha ya Kiswahili kuna utata unaosababisha na miundo ya virai kisemantiki. Mfano: juma hamthamini rafiki yake mwanahawa Juma amempigia annet mpira. Ni dhahiri kuwa kisemantiki kuna utata, kwani kuna maana Zaidi ya moja katika sentensi hizo hapo juu, kwani katika sentensi ya kwanza tunaweza elewa kuwa ; Mwanahawa ndiye hathaminiki au Rafiki yake na mwanahawa ndiye hathaminiki. Ushahidi wa kisintaksia:Ushahidi huu unaonyesha mtawanyo wa virai. Hii inamaana kwamba ukitaka kuhamisha maneno yaundayo virai, hauna budi kuhamisha kirai kizima na si sehemu tu ya kirai hicho, kudondosha au kuunganisha kirai kizima Mfano: simuwezi dada yako mkubwa. Dada yako mkubwa simwezi. Simpendi kaka yako mkorofi. · Mkubwa simwezi dada yako. · Mkorofi kaka yako simpendi. Kuunganisha virai vyenye hadhi sawa. Mfano: i) baba analima Mama analima Baba na Mama wanalima. ii) John anasoma kiti kimevunjika John na kiti vimevunjika/wanasoma Sentensi II, hazijaleta maana kwa sababu hadhi siyo sawa an sentensi si sahihi. Vile vile katika ushahidi wa kisintaksia kuna jaribio la kiubadala (replacement) kulingana na baadhi ya wanaisimu akiwemo carnie Andrew(2007)na O’graddy(1996:193-194) wanasema: Jaribio la kiubadala hujidhihirisha pale baadhi ya maneno huweza kusimama badala ya kirai kizima au kundi la maneno hususani katika kirai nomino na kirai kitenzi ambavyo vinaweza kuwakilishwa na viwakilishi na maneno kama hivyo au hivyo hivyo n.k. Mfano: i) wanafunzi watavai tai endapo walimu nao watavaa Ubadala; Wanafunzi watavaa tai endapo walimu watafanya hivyo ii) wanafunzi watakao soma kwa bidii watafaulu mitihani vizuri ubadala: wao watakaosoma kwa bidii watafaulu mitihani vizuri Kwa hiyo si kweli kwamba hakuna kategoria ya virai katika uchanganuzi wa kisintaksia. Kuna kategoria ya virai, na virai hivyo vimejikita Zaidi katika neno kuu ambalo kuna aina mbalimbali za virai ambavyo ni kirai nomino, kirai kivumishi, kirai kitenzi, kirai kielezi, kirai kibainishi na kirai kihusishi. Ufuatao ni uchanganuzi wa virau Kisintaksia. 1. KIRAI NOMINO. Ni kirai ambacho muundo wake umekitwa kwenye nomino au mahusiano ya nomino na neno au mafungu ya maneno. Miundo ya nomino: i)Nomino peke yake. Mfano: Dada ameondoka N Juma atarudi kesho. N KN N Dada/Juma ii) Nomino mbili. Mfano. Baba na mama wanalima. N1 N2 KN N u N2 Baba na mama iii) Nomino na Kivumishi kimoja au Zaidi. Mfano: Watu watatu warefu wamesimama njiani. N KN N KV V KV V Watu Watatu Warefu iv) Nomino na kirai kibaishi Mfano: Mwanafunzi yule anacheza KN KN N KB B Mwanafunzi yule v) Nomino na sentensi Mfano: Mtoto aliyepotea jana ameonekana. KN N S KN KT N T KE Mtoto aliyepotea jana Vi) Nomino, kivumishi na sentensi. Mfano:a) msichana mrembo aliyehamia jana amekwenda sokoni. b) John mrefu aliyekwenda sokoni asubuhi amepata ajali. KN N KV V S KN KT N T KE E Msichana Mrembo aliyehamia jana vii) nomino, Kibainishi na sentensi mfano:a) watoto wengi wanaofaulu masomo ni wanao soma kwa bidii. b) vijana wengi wanasiofaulu hawasomi sana KN N KB S B KN KT N T KE E1 E2 Vijana wengi wasiofaulu mitihani yao 2. KIRAI KIVUMISHI. Ni kirai ambacho muundo wake umekitwa katika kivumishi kwa kawaida muundo huo huwa ni wa kivumishi na neno au fungu la maneno linaloandamaana na kivumishi hicho. Ifuatayo ni miundo ya kirai kivumishi. a) Kivumishi pekee yake. Mfano: kiti kizuri Mtoto mzuri Kijana mbaya KN V Kizuri Mzuri b) kivumishi na kirai nomino. Mfano: i) mtoto mwenye kelele nyingi ii)Mwanafunzi mchafu miguu yake KV KV KN N KB B Mwenye kelele nyingi c) kivumishi na kirai kielezi. Mfano: a)Chungwa baya sana. b)Mama korofi sana. c) Mwalimu mpole mno. KN V KE E Mpole mno d) kivumishi na sentensi. Mfano: motto mzuri aliyekuja sana asubuhieondoka. Maji machafu yaliyotiririka mferejini yananuka. KN V S KN KT N T KE E Machafu yaliyotiririka mferejini e) kivumishi na kirai kihusishi, mfano: mme mzuri wa dada anaumwa. Kilio kikubwa cha watanzania ni maji safi KV V KH H KN N Kikubwa cha watanzania f) Kivumishi na kirai kivumishi mfano; Simu nzuri nyeusi imeibiwa Ua zuri jekundu limenyauka KV V KV V Zuri jekundu 3.KIRAI KITENZI Ni kirai ambacho mahusiano ndani yake yamekitwa katika kitenzi (Kihore na wenzake 2007) ni kirai ambacho kimekitwa katika kitenzi, hii ina maana kuwa neno kuu katika aina hii ya kirai ni kitenzi(Massamba na wenzake 2009) Miundo ya virai vitenzi ni kama ifuatavyo a) Kitenzi peke yake mfano; Amelala ;Wameamka KT T Amelala b) Kitenzi na nomino moja mfano; amempiga juma ameandika barua KT T KN N Ameandika barua c) Kitenzi na nomino mbili. Mfano; amempa motto chakula Wanampigia juma kelele KT T KN N1 N2 Amempa mtoto chakula d) Kitenzi na kitenzi, mfano; anapenda kutoa ameamua kurudi anapenda kusoma KT T1 T2 Anapenda kutoa e) kitenzi, nomino na kitenzi. Mfano: anamfundisha mototo kusoma Tuliwataka viongozi kututembelea KT T KN N KT T Anamfundisha motto kusoma f) kitenzi na sentensi mfano: amesema atarudi kesho KT T S KN KT N T KE E Amesema atarudi kesho g) kitenzi na kirai kihusishi mfano: ameondoka kwa basi anatembea kwa baiskeli KT T KH H KN N Anaondoka kwa baiskeli h) kitenzi, nomino na sentensi mfano: mwalimu amewambia wanafunzi waende darasani KT T KN N S KN KT N T KE E Amewambia wanafunzi waende darasani 4. KIRAI KIELEZI Kirai kielezi ni aina ya kirai ambacho kwacho neno kuu ni kielezi. Kirai hiki kinaweza kuwa na neno kuu peke yake au kikaambatana na kijalizo chake. Miundo ya kirai kielezi ni kama ifuatavyo: a) kirai kielezi peke yake mfano: jane analimima shambani peter ameweka kiti chini KE E Shambani b) kielezi na kielezi kingine mfano:William anaimba vizuri sana boom limetoka leo asubuhi KE E KE E Leo asubuhi C) kielezi na kirai kihusishi Mfano: mototo anakula nyumbani kwa watu Alicheka kwa sauti mkutanoni KE E KH H KN N Nyumbani kwa watu 5 .KIRAI KIHUSISHI; Hii ni aina ya kirai ambayo neno kuu ni kihusishi, mara nyingi kirai kihusishi hakiwezi kuwa na muundo wa kihusishi peke yake hivyo hulazimika wakati wote kuhitaji kijalizo ili kukamilisha maana yake. Mfano: anazungumza kuhusu mavazi Juma anakula kuku kwa mrija Wazurulaji wamekamatwa na polisi. Miundo ya kirai kihusishi ni kama ifuatavyo: a) kirai kihusishi na nomino mfano: amezungumzia kuhusu mavazi KH H KN N Kuhusu mavazi b) kirai kihusishi na kitenzi mfano: jane ameadhibiwa kwa kuimba juma alipongezwa kwa kufaulu KH H KT T Kwa kufaulu c) kihusishi, nomino na kivumishi mfano :nimechoka kwa matusi yake ameolewa kwa bwana mzuri KH H KN N KV V Kwa bwana mzuri d) kihusishi, nomino na kibainishi mfano: wanapendana katika hali zote mababu zetu waliishi katika bara hili KH H KN N KB B Katika hali zote 6.KIRAI KIBAINISHI: Kirai kibainishi ni aina ya kirai ambayo ni neno kuu huwa ni kibainishi na huweza kuwa peke yake au kuambatana na kijalizo chake. Miundo ya kirai kibainishi: a) kibainishi peke yake mfano :anauza gari lile mama anafuga ng’ombe wawili KB B Wawili b) kibainishi na kivumishi mfano: kajifungua watoto wawili wazuri amenunua mbuzi wane wanene KB B KV V Watatu wanene c) kibainishi na kibainishi kingine mfano: viwanja hivi viwili ni mali yangu KB B KB B Hivi viwili d) kibainishi na sentensi mfano: mwalimu amewafundisha wanafunzi wale waliokuwa hawajaelewa kaka yule aliyeigiza na kanumba ni mpare KB B S KN KT N T1 T2 Wale waliokuwa hawajaelewa Hivyo basi ni dhahiri kuwa kuna kategoria za virai katika uchanganuzi wa kisintaksia katika lugha ya Kiswahili kwani kwa ushahidi na ubainishaji wa aina mbalimbali za virai na miundo yake twaweza sema kuwa hizi kategoria zipo. MAREJEO: Massamba P.B na wenzake (2009) sarufi miundo ya Kiswahili sanifu (SAMIKISA): sekondari na vyuo, TUKI, Dar es salaam. Kihore M. Y na wenzake (2007) sarufi maumbo ya kiswahili sanifu (SAMIKISA): sekondari na vyuo,TUKI, Dar es salaam. TUKI (2011) kamusi ya Kiswahili sanifu. TUKI, Dar es salaam. Andrew .C. (2007) syntax: a generative introduction second edition; blakwell publishers LTD.USA. O’graddy .W. (1996) syntax: The analysis of sentence structure; Longman limited. London Give Your Comment

No comments:

Post a Comment