Saturday

UMESIKIA ALICHOAMBIWA BOCCO ?

0 comments


MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Simba, Mussa Hassan Mgosi amemshauri mshambuliaji wa sasa wa klabu hiyo, John Raphael Bocco aongeze mazoezi ili awe fiti zaidi aweze kung’ara Msimbazi.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mgosi amemuambia Bocco kwamba anaweza kuwa mchezaji muhimu iwapo tu ataongeza bidii ya mazoezi na kuwa fiti zaidi.
“Asante kijana wangu, mimi ninajua kwa aina yako wewe ni mchezaji unayehitajika sana Simba, ongeza feetness ili wengine nao waamini hiki ninachokiamini mimi,”aliandika Mgosi.
Na Mgosi aliyewahi pia kuchezea Mtibwa Sugar ya Morogoro, JKT Ruvu ya Dar es Salaam na Daring Club Motema Pembe (DCMP) ya Kinshasa aliposti ujumbe huo ulioambatana na picha ya Bocco baada ya mchezaji huyo kuifungia Simba bao pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons Jumamosi iliyopita Mbeya.