Wednesday

Watu 150 wafariki kwa ugonjwa usiojulikana nchini Nigeria

0 comments

Watu  150 waripotiwa kufariki katika jimbo la Kano  kwa maradhi yasiojulikana nchini Nigeria.

Mkurugenzi wa hospitali ya mafunzo ya udaktari  Aminu Kano,  Isa Abubakar   amefahamisha kuwa watu  150 wamekwishafariki  kwa maradhi ambayo hayajajulikana  nchini humo.

Mkurugenzi huyo amesema kwamba vifo hivyo vimetokea kati ya Ijumaa na Jumapili wiki iliopita.

Daktari Isa Abubakar amefahamisha kuwa watu waliofariki ni watu wenye umri wa kuanzia miaka  60.

Daktari huyo amewaambia wanahabari kuwa  huenda watu hao wamefariki  kwa virusi vua corona kwa kuwa sio jambo la kawaida idadi kubwa ya watu kufariki kwa mkupuo.

Nchini Nigeria ni watu  22 ndio  wamekwishafariki kwa virusi vya corona na wengine  665 wakiwa wamekwishaathirika na virusi hivyo.

No comments:

Post a Comment