Monday

Matumizi ya nadharia ya vijenzi-semantiki katika uchambuzi wa melonimia katika lugha ya kiswahili

0 comments

 

 

 

Lugha ya Kiswahili

 

Matumizi ya Nadharia ya Vijenzi-Semantiki katika Uchambuzi wa Meronimia katika lugha ya kiswahili


Na,

 Hashim Juma

(2020-06-01628)

Ikisiri

Makala haya yamenuia kuangazia matumizi ya Vijenzi-Semantiki katika uchambuzi wa 

meronimia. Meronimia ni uhusiano uliopo baina ya leksimu inayotaja sehemu na ile inayotaja 

kitu kizima (taz, Matinde, 2012: Resani, 2014: Kahigi, 2019). Okal (2018), Okal na wenzake 

(2017) wamejaribu kutumia Nadharia ya Vijenzi-Semantiki kwenye uchanganuzi wa hiponimia 

hususani kwenye nomino. Pamoja na hiyo nadharia kutumika katika uchanganuzi wa hiponimia 

inaaminiwa kuwa Nadharia ya Vijenzi-Semantiki inaweza kutumika katika uchanganuzi wa 

meronimia. Suala Hili linashadadiwa na Okal (2018). Licha ya nadharia ya vijenzi-semantiki 

kusadikika kwamba inaweza kutumika kuchanganua meronimia, hakuna utafiti ambao 

umeonesha jinsi nadharia ya vijenzi-semantiki inavyoweza kutumika kuchanganua meronimia 

mbali na hizo zilizotumia Hiponimia. Hivyo makala haya yamekusudia kuonesha matumizi ya 

vijenzi semantiki kwenye kuchanganua meronimia. 

1.0 Utangulizi

Makala haya yanafafanua matumizi ya vijenzi-semantiki katika uchambuzi wa meronimia. 

Lengo la makala haya ni kuonesha namna ambavyo nadharia ya vijenzi-semantiki inavyoweza 

kutumika kufanya uchambuzi wa meronimia. Nadharia ya vijenzi-semantiki aghalabu hutumika 

kwenye uchambuzi wa hiponimia, hata hivyo inaweza kutumika kwenye uchambuzi wa 

meronimia kwa kuwa zote zina sifa ya udarajia.





Pakua makala hii yote kwa kubofya hapa


👉🏾👉🏾https://drive.google.com/file/d/1-AICIxWnixZ8lqjjXkmhX80DwOKh0BnG/view?usp=drivesdk

No comments:

Post a Comment