Wednesday

Watu 10 wafariki katika ajali ya ndege Russia Boss wa Wegner atajwa

0 comments

 


Watu 10 wamekufa baada ya ndege binafsi iliyokuwa ikitokea Moscow kuelekea St. Petersburg kuanguka.

Vyombo vya habari vya Urusi na maafisa wa anga wamesema kuwa mwanzilishi wa kundi binafsi la kijeshi la Urusi la Wagner, Yevgeny Prigozhin alikuwa kwenye orodha ya abiria wa ndege hiyo. 

Hata hivyo haijafahamika mara moja kama alikuwa ndani ya ndege hiyo. Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinaeleza kuwa ndege hiyo ni mali ya Prigozhin, ambaye aliongoza uasi mwezi Juni dhidi ya jeshi la Urusi.

No comments:

Post a Comment