Saturday

UHAKIKI RIWAYA YA FIRAUNI SEHEMU YA TATU

0 comments

Firauni ni riwaya mpya iliyotoka hivi karibuni. Upya wa riwaya hii si tu kwa sababu imechapishwa hivi karibuni, la hasha! Bali ni kwa sababu ya upya wa mawazo yake  ambayo yanasawiri barabara matukio anuwai yatokeayo katika jamii zetu wakati huu. Riwaya hii iliandikwa na mpenzi wa Kiswahili Athumani Mauya  inatugusa sisi Watanzania na pia watu wa jamii nyingine za Kiafrika kwa sababu ya uhalisia na uzito wa matukio yanayojadiliwa na mwandishi huyu Athumani Mauya.  


Akiwa Dar es Salaam  alikutana na msichana  mrembo aliyejulikana  kwa jina la  Kunguru  ambaye  alikuwa amelelewa na  katika maadili, mpole, mwenye heshima na adabu, mkweli asiye na hatia. Buna aliamua  kumuoa binti huyo.
Wakati wa kupima afya zao kabla ya kuoana  Buna alikula njama  na daktari  ili majibu ya damu yatoke kwa matakwa  ya mashine. Buna laifariki dunia kwa Ukimwi akiwa mikononi mwa  Kunguru na kumwacha na msongo wa mawazo na mfadhaiko mkubwa asijue la kufanya huku ndugu zake Buna wakitaka kumdhulumu mirathi.


Info.masshele@gmail.com
Firauni ni riwaya mpya iliyotoka hivi karibuni. Upya wa riwaya hii si tu kwa sababu imechapishwa hivi karibuni, la hasha! Bali ni kwa sababu ya upya wa mawazo yake  ambayo yanasawiri barabara matukio anuwai yatokeayo katika jamii zetu wakati huu.
Riwaya hii iliandikwa na mpenzi wa Kiswahili Athumani Mauya  inatugusa sisi Watanzania na pia watu wa jamii nyingine za Kiafrika kwa sababu ya uhalisia na uzito wa matukio yanayojadiliwa na mwandishi huyu Athumani Mauya.
Firauni ni riwaya inayoangaza baadhi ya watu katika jamii. Riwaya hii imejikita zaidi katika michezo michafu  inayochezwa katika sehemu za kazi na katika jamii kwa jumla, husasan dhidi ya wanawake.
Maovu hayo ni pamoja na ufisadi, uonevu, dhuluma, uasherati na usambazaji wa virusi ya Ukimwi kwa makusudi. Mengine ni ukandamizaji wa wanawake na wajane hususan katika mirathi, ushirikina, hujuma serikalini, rushwa ya fedha, rushwa ya ngono na upendeleo katika sehemu za kazi na mahali pengine.
Maovu hayo yanajionyesha wazi katika matendo anayotenda mhusika Buna na wenzake . Buna mwenye shahada ya uzamili alianza kazi katika kampuni ya kuchonga vinyago  akiwa maskini wa kutupwa kiasi kwamba  hata mlo wake ulikuwa wa shida. Aliishi kwa kuombaomba na kukopa.
Maisha ya Buna yalibadilika  baada ya kwenda likizo kijijini kwao. Huko alikutana na Dube ambaye alikuwa Naibu Waziri.
Dube aliwenda kule kijijini kwa mganga maarufu  wa jadi aitwaye  Dunga, mjomba wake Buna kwa ajili ya kuroga  ilia apate mafanikio kazini  kwake. Mfafanikio hayo  ni kutokufukuzwa kazi, kushinda ubunge,  na kuwa waziri kamili.
 Baada ya Dube kufanikiwa  katika azma yake akajenga uhusiano mzuri na  na Buna. Ili kupata hisani  kwa Dunga, Dube akafanyia mpango Buna kuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Usafi  na Mazingira (Tauma) huko Arusha. Mara baada ya kupata wadhifa huo, Buna alianza kushirikiana na  Mhasibu wa Tauma  wakaanza kuiba fedha za taasisi na kufanya hujuma mbalimbali. Aidha, akaanza tabia ya uasherati  ndani na nje  ya ofisi kiasi  kwamba baadhi ya makahaba wake walikuwa wakija ofisini kwake kufanya fujo hata kupigana  na kuharibu nyaraka za serikali.
Kutokana na tabia yake ya uasherati  aliokuwa akiuendeleza  alipata maambukizo ya ugonjwa wa Ukimwi yaliyosababisha kifo cha mkewe. Juma moja baada ya mkewe kufariki dunia, Buna alipata barua ya kuachishwa kazi kwa manufaa ya umma. Akaondoka Arusha kwenda Dar es Salaam kuwa mfanyabiashara.
Akiwa Dar es Salaam  alikutana na msichana  mrembo aliyejulikana  kwa jina la  Kunguru  ambaye  alikuwa amelelewa na  katika maadili, mpole, mwenye heshima na adabu, mkweli asiye na hatia. Buna aliamua  kumuoa binti huyo.
Wakati wa kupima afya zao kabla ya kuoana  Buna alikula njama msichana, Buna, maadili,heshime,  uahserati,  na daktari  ili majibu ya damu yatoke kwa matakwa  ya mashine. Buna laifariki dunia kwa Ukimwi akiwa mikononi mwa  Kunguru na kumwacha na msongo wa mawazo na mfadhaiko mkubwa asijue la kufanya huku ndugu zake Buna wakitaka kumdhulumu mirathi.
Katika mazingira hayo ya kutaka kudhulumiwa, akajitokeza msichana  aliyepambana na wazee wa ukoo na wanaume  kuhakikisha kwamba  Kunguru anapata haki yake. pamoja na maneno ya laana  na vitisho, Hidaya hakujali kitu.
Hii ni riwaya yenye uhalisia wa jamii yetu. Shime tuisome!
Mwisho.

No comments:

Post a Comment