Saturday

MUUNDO NA UMBO LA USHAIRI

0 comments




Katika umbo wa shairi, tunaangazia jinsi shairi lilivyoundwa kwa kuangazia mizani, vina, mishororo n.k Aidha, ni muhimu kutaja aina na bahari za shairi zinazohusiana na kila sifa uliyoitaja.
  1. Idadi ya mishororo katika kila ubeti - Tumia idadi ya mishororo kubainisha aina ya shairi hilo. 
  2. Kwa mfano: Shairi lina mishororo minne katika kile ubeti, kwa hivyo ni Tarbia
  3. Idadi ya mizani katika kila mshororo na katika kila kipande cha mshororo. 
  4. Kwa mfano: Kila mshororo una mizani kumi na sita: nane katika utao na nane katika ukwapi.
  5. Idadi ya vipande katika kila mshororo - Taja ikiwa shairi lina kipande kimoja, viwili, vitatu au vinne kisha utaje bahari yake.
  6. Kituo, kiishio au kibwagizo - Ikiwa mstari wa mwisho umerudiwa rudiwa, basi shairi lina kibwagizo aukiitikio, la sivyo lina kiishio.
  7. Vina - Zingatia vina vya kati na vya mwisho kutoka ubeti mmoja hadi mwingine. Kisha utaje ikiwa niMtiririko, Ukara au Ukaraguni

No comments:

Post a Comment