Mkuu wa wilaya ya Kaliua, Paul Chacha amewasimaisha kazi watumishi wawili wa hospitali ya wilaya hiyo kwa tuhuma za kushiriki mapenzi hovyo wodini.

Chacha amesema awali ulifanyika uchunguzi baada ya wagonjwa kulalamikia vitendo vya wauguzi hao kufanya mapenzi wodini wakiwa zamu za usiku.

Mmoja wa wahudumu hao alikuwa kwenye mafunzo ya vitendo na mwenzake alikuwa ni mtumishi wa hospitali hiyo.

Chanzo : CG Fm

======

Siku chache baada ya mganga wa Hospitali ya Wilaya ya Kaliua, Irene Apina kusimamishwa kazi kwa tuhuma za kukataa kumpa matibabu mtoto wa miaka mitano, wauguzi wawili wa hospitali hiyo wamesimamishwa kazi kwa vitendo vya utovu wa nidhamu.

Watumishi hao, mmoja anatuhumiwa kufanya mapenzi wodini na daktari ambaye yupo katika mafunzo kwa vitendo huku mwingine akituhumiwa kuwa kinara katika utoaji wa mimba.

Katika kikao chake na watumishi wa sekta ya afya, Mkuu wa Wilaya ya Kaliua (DC), Paul Chacha aliwasimamisha kazi watumishi hao na kila mmoja kumpa tuhuma zake.

DC Chacha amesema kuwa baada ya kuwasimamishwa kazi, tayari kuna timu imeundwa kuchunguza tuhuma zao.

Amesema kuwa muuguzi wa afya katika hospitali hiyo ambaye jina limehifadhiwa anatuhumiwa kwa kuwa kinara wa utoaji mimba huku mhudumu wa afya akilalamikiwa na wagonjwa kufanya mapenzi wodini na daktari ambaye yupo kwenye mafunzo.

"Kama huyu mtu ni daktari akiwa mafunzoni maana yake ndio kipindi cha matazamio halafu bado mnamuacha hapo anafanya nini? Taarifa yake iende mbaya kuwa hafai" amesema Mkuu huyo wa Wilaya

Daktari huyo aliye mafunzoni anatuhumiwa kufanya mapenzi wodini ambapo inadaiwa wagonjwa wamekuwa wakikerwa na kitendo hicho na kuanza kulalamika.

Mkuu huyo wa wilaya amesema hataki kuona mambo yasiyofaa katika Wilaya anayoiongoza na kwamba hatasita kuchukua hatua stahiki lengo ni kukomesha tabia mbaya na watumishi wawe mfano kwa kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mwananchi