Tuesday
Breaking: Matokeo ya mitihani ya kitaifa KCPE (KENYA CERTIFICATE OF PRIMARY EDUCATION )
Matokeo ya mtihani KCPE RESULTS 2022/2023
Waziri wa elimu Ezekiel Machogu ametangaza wazi kuwa matokeo ya mitihani ya darasa la nane KCPE yatatangazwa wiki kesho.
Machogu alisema kuwa wizara yake imeweka mikakati kabambe ya kuhakikisha kuwa hakuna visa vya wizi wa mitihani ya kitaifa ya sekondari KCSE ambayo inaendela kote nchini.
Machogu alikuwa akiyazungumza haya wakati wa hafla moja ya mazishi eneo bunge la Nyaribari Masaba ambapo alikuwa mbunge kabla ya kuwania ugavana wa kaunti ya Kisii katika uchaguzi uliopita wa Agosti 9.
“Wiki ijayo tunatangaza matokeo ya mtihani wa KCPE na hutasikiliza kesi zozote za udanganyifu chini ya uongozi wa Machogu. Upangaji wa alama za Cheti cha Elimu ya Sekondari cha Kenya (KCSE) unaendelea vyema na ninakuhakikishia, matokeo hayatakuwa na dosari zozote,” alisema waziri Machogu.
Mitihani ya KCPE ilikamilika mwanzoni mwa mwezi wa Desemba ambapo ni takribani wiki moja na siku kadhaa.
Matokeo hayo yatatoka siku chache tu kuelekea sherehe za Krismas, wakati ambapo mitihani ya kidato cha nne itakuwa inakamilika pia kote nchini.
KCSE iling’oa nanga mwanzoni mwa mwezi hu wa Desemba kwa wiki tatu hadi tarehe 23 Desemba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)