ELEZA KWA KINA DHANA
ZIFUATAZO:
1) Usuli
Usuli
wa utafiti ni kile ambacho kimempa msukumo mtafiti kuifanya kazi yake. Waaidha
huwa ni maelezo mafupi yanayohusu historia fupi kuhusu suala la utafiti ambalo
unanuia kulifanyia utafiti.
Kwa
mfano ikiwa mtafiti angenuia kufanya utafiti kuhusu sababu za wanafunzi wa eneo
la pwani kutoweza kufanya vizuri katika somo la Kiswahili kwenye mtihani wa
kitaifa, basi mtafiti husika hana budi kuyafafanua haya kuhusu Usuli wa utafiti
wake kuhusu mada yake:
Kiswahili
ni mojawapo ya lugha za mawasiliano nchini Kenya, ikiwa lugha rasmi ya kitaifa.
Kuna malalamishi kuwa chimbuko la lugha ya Kiswahili ni upwa wa Afrika
Mashariki (Massamba 2001), likiwemo eneo la Mkoa wa Pwani, nchini Kenya.Tume ya
Elimu ya Gachathi 1976, ilipendekeza kuwa Kiswahili liwe somo la lazima kisha
litahiniwe katika shule za msingi na za upili.
Nayo
Tume ya Elimu ya Mackay 1981, ikatekeleza pendekezo la Tume ya Elimu ya
Gachathi 1976 katika mfumo wa elimu wa 8-4-4. Kufikia sasa, ni zaidi ya miongo
miwili tangu Kiswahili kilipoanza kutahiniwa katika kiwango cha kitaifa, kukiwa
bado kuna madai kwamba matokeo ya mitihani ya Kiswahili ya K.C.P.E na K.C.S.E
yamekuwa mabaya na yanaendelea kuwa mabaya. “Matokeo ya wanafunzi katika
Kiswahili hayaridhishi. Kazi ya wanafunzi hasa katika insha za Kiswahili
ilionyesha tofauti ndogo sana kutoka kwa ile ya mwaka wa 1989.”
Katika
Usuli mtafiti anaweza vile vile kurejelea utafiti wa Mashirika au watu
mabalimbali kama Kichocheo cha kumwezesha kuufanya utafiti wake.Kwa kulishughulikia
hilo huwa ni ithibati tosha kuwa mtafiti anafahamu panda-shuka zote katika
uwanja anaotarajia kutafiti.
2) Swala la utafiti.
Hili
huwa ndiyo mada au pengo ambalolinatarajiwa kuzibwa katika utafiti husika.
Kwa nini kuwe na swala la utafiti?
-
Ikiwa
watu wanazidi kuongelea juu ya swala hilo.
-
Kwa
kuiangalia tu kama mtafiti.
-
Hutokea
pale ambapo mtu binafsi au kiwanda Fulani kinazidi kuwa na matatizo
-
Mada
ya utafiti hutokea plale ambapo kuna njia mbili ambazo zinahitajika kusuluhisha
shida/tatizo hilo.
JINSI YA KUTEUA MADA YA UTAFITI
Mugenda na
Mugenda, Research Methods (1999)
wanasema mchakato wa utafiti huanza kwa kuchagua mada ya utafiti na hili huwa
jambo tata kwa wanafunzi na hata watu ambao wamebobea katika uwanja huu wa
utafiti.
Swali
unalopaswa kujiuliza ni je nataka kutafiti kuhusu jambo gani? (Hiyo ndiyo mada)
hii ni kwa sababu mada kamilifu yapaswa kujitosheleza na kulenga tatizo maalum
lenye mipaka halisi. Haifai iwe pana wala finyu bali iwe wastani mada pana
hulenga mambo mengi na hivyo huleta matatizo katika utekelezaji wakati
unapofanya utafiti.
Isitoshe,
matokeo yake pia hayashuluhishi tatizo lolote maalum kwa sababu yana ugumu wa
kupima utabiti na udhaminifu wake kuambatana na vigezo vya utafiti. Vilevile,
mada finyu pia haistahili (si mwafaka) kwa sabau haitakupa matokeo ya
kuridhisha kwa hivyo mada nzuri ya kifanyiwa utafiti ni mada wastani. Mtafiti
anaweza anza kwa kuchagua mada pana kisha aivunje hadi apate mada wastani.
Mifano:
(a)
Athari ya dawa za kulevya nchini Kenya
(b)
Athari
ya dawa za kulevya kwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Kenyatta
(c)
Athari
za dawa za kulevya katika wanafunzi wa darasa la nane chuo cha Kenyatta
Katika (a)
Kenya ni kubwa na ina kaunti nyingi anayeiona mada hii atajiuliza ikiwa mtafiti
ataweza kusanya data nchi nzima, kwa wakati ufaao pia gharama itakuwa ghali
vile vile wanafunzi wa darasa la nane ni wachache matokeo hayatakuwa ya
kuridhisha. (b) Ndiyo mada wastani, kwa hivyo uzingatie ikiwa mada
utakayochagua itakuelekeza kuyafikia matokeo au la ikiwa jibu lako ni la
(i)
Achilia
mbali mada hiyo na utafute nyingine
(ii)
Irekebishe
kwa kuifungia katika mipaka maalum itakayokusaidia kazi yako vyema.
Kulingana na
Charlotte S. W. na Ryanga A. (2002). Unaweza kutambua mada mbaya isiyoweza
kutafitika, ama kuwa na suluhisho mwafaka kwa kuzingatia vidokezo hivi:
- Ikiwa ni pana mno na haizingatii swali maalum
- Ikiwa inashughulikia tatizo lisilo na suluhisho
linalobainika
- Ikiwa utafiti huo hautajaza pengo lililoachwa na
watafiti wengine katika uvumbuzi wao ama kuthibitisha au kukanusha kigezo
kipya cha nadharia.
Kwa ajili ya
utaratibu unaohusu utafiti, wataalamu wa utafiti Barzun na Graff (1957)
walisema: kusoma, kuandika na kutafakari ni mambo matatu muhimu. Katika
shughuli ya utafiti mtafiti atafakari na kuchunguza mada yake ili afahamu dhana
zote zilizopo.
UUNDAJI WA SWALA LA
UTAFITI
Katika uundaji wa swala la utafiti hatua zifuatazo huzingatiwa
(i)
Mahitaji ya mada ya utafiti/(urgency).
(ii)
Umuhimu
wa mada hiyo kwa jumla, mada hiyo inawaathiri watu gani, kwa kiwango gani na
kwa kiasi kipi?
(iii)
Gharama
na vitu vingine ambavyo vitaweza kukamilisha mada hiyo.
(iv)
Utumikaji,
mapendekezo ya utafiti yanaweza kutimika?
(v)
Usitafiti
mada zilizofanyiwa utafiti tayari.
(vi)
Chunguza
usije ukawa unamwathiri mtu yeyote katika utafiti.
(vii)
Ni
bora kutafiti kuhusu mada ambayo huungwa mkono na watu walio na mamlaka.
Hatua za Kuchagua swala la utafiti.
Kuna mambo
kadha yatakayo kupatia mada ya utafiti. Yaweza kutokana na:
- Nadharia zilizopo (existing theories)
- Tajriba ya maisha ya jamii
- Kadhia na harakati za maisha
- Utafiti uliotanguliwa kufanywa (previous research
studies and relications)
- Tajriba ya mtu (personal experience)
- Kongamano na majarida mbalimbali (discussion with
experts)
- Vitabu, tasnifu na majarida mbalimbali (books, theses
and other written materials)
- Vyombo vya habari (assertions from the media)
- Maoni na mapendekezo ya wataalam, halmashauri ya
watu wa ngazi za juu .
(i) Nadharia zilizopo
Nadharia ni
kundi la sheria zilizopangwa katika utaratibu na mfumo maalum. Ni muhtasari wa
muingiliano na uhusiono wa ujuzi wa kijumla ambao tayari upo. Husaidia kuzua
jambo la kutafitiwa. Pia humuongoza mtu kwenye masuala ya utafiti ikiwa mada
inayoshughulikiwa imejikita katika misingi ya kinadharia.
(ii) Kadhia na harakati
za maisha
Kila jamii ina
visa mbalimbali na hali wanazokabiliana nazo kila wakati. Kama magonjwa,
uhusiano, matumizi ya lugha magazetini na muingiliano wa tamaduni mbalimbali.
Haya yote hudhihirika katika taathira mbalimbali. Wakati mwingine mambo haya
hujadiliwa katika ngazi ya kitaifa na swala lako laweza kutokana na mambo kama
haya.
(iii) Utafiti wa Awali
Ripoti za
tafiti zilizofanywa awali huelezwa katika sura ya mapendekezo ambapo mtafiti
anayetamatisha kazi yake bado anaona utafiti zaidi unahitajika. Uchunguzi zaidi
ukifanywa huongeza ujuzi na ubora wa kazi hiyo. Pia mtafiti huweza kuchunguza
jinsi nadharia fulani ilivyotumika na akubaliane au asikubaliane nayo kwa
kuondoa utata unaoleta ubishi. Anaweza kuonyesha kuwa nadharia haikufaa katika
kazi ile hivyo atachukua ripoti hii na kuifanya msingi wa suala lake la
utafiti.
(iv) Tajriba ya Mtu Binafsi
Suala la
utafiti linaweza kutokana na mambo ambayo mtafiti mwenyewe ameshuhudia. Mfano:
mtu aliyenusurika katika mkasa wa Westgate anaweza kufanya utafiti kuhusiana na
usalama au jinsi serikali ilivyotayari katika kukabiliana na vita kama hivi.
(v) Kongamano na Mijadala ya Wataalamu
Mjadala na
kongamano ya wataalamu kuhusu mambo yanayotendeka kwa wakati huo na kutokana na
warsha au mikutano kama hiyo, mtafiti akihudhuria huweza kupata mada ya utafiti
kwa sababu wanaoshiri katika mikutano hiyo ni watu waliobobea katika nyanja
hiyo.
(vi) Vitabu, tasnifu na majarida mbalimbali
Unaweza kupata
suala lako la utafiti kwa kusoma vitabu vilivyoandikwa na wataalamu mbalimbali.
Unaposoma unapata mwanga na kutambua suala la utafiti, kusoma zaidi ni
kuelimika zaidi.
(vii) Vyombo vya Habari
Kuna mambo
mengi yanayoendelea katika vyombo vya habari taarifa, mijadala na habari
zinazochapishwa kila uchao, haya yote yanaweza kumwezesha mtafiti kutambua
suala lake la utafiti.
(viii) Maoni na mapendekezo ya wataalamu, halimashauri na
watu wa ngazi za juu
Haya ni mambo
au mitazamo mbalimbali ya watu wenye ushawishi katika jamii kuhusu maswala
fulani yanayohitaji kufanyiwa utafiti haswa hapa nchini Kenya. Mfano katiak
idara ya usalama hapa nchini Kenya.
Vipimio vya swala la
utafiti
1.
Uhalisia, uzito na ueneaji wa mada ya utafiti
-
Ukubwa
na utokeaji wa mada ya utafiti. Yaani hutokea mara kwa mara, kwa kiwango kipi?
Na unathiri vipi na mathara yapi huletwa na mada hiyo ya utafiti?
2.
Nini
kinachosababisha utokeaji na uendeleaji wa mada hiyo ya utafiti. Chunguza
kwanza zile sababu ambazo husababisha tatizo hilo.
3.
Fafanua
kwa nini wataka kufanya utafiti
4.
Elezea
mkutadha ambao mada ya utafiti hutokea.
Hatua za uanishaji wa mada ya utafiti
1.
Kueleza mada ya utafiti kwa ujumla.
2.
Kuelewa
uhalisia ambao unatokea.
3.
Kutembela/kurejelea
makisio ya maandishi yanayopatikana.
4.
Kufafanua
mada ya utafiti.
5.
Kueleza
mkutadha inamotokea.
6.
Buni
nadharia tete, maswali ya utafiti n.k
Sifa za Mada Nzuri ya Utafiti
Christensen L.
B. (1985) (Experimental Methodology)
Anasema kuwa
suala nzuri la utafiti lisilo na utata husaidia kwa kudhihirisha aina ya vifaa
vya kukusanya data, aina ya data inayokidhi upimaji wa nadharia tete na mbinu
mwafaka za uchunguzaji wa data. Hii ina maana kuwa mada nzuri lazima ikuongoze
kwa vyovyote vile.
Hizi ni baadhi
ya sifa za mada mwafaka
- Ilenge tatizo maalum ambalo ndilo pengo linalofaa
kushughulikiwa
- Ikuongoze katika kupata suluhu kwa tatizo hilo na
suluhu hilo liwe la kuleta faida
- Iwe na upeo na mipaka maalum
- Ieleweke kwa urahisi
- Uwezekano hasa katika upeo na mipaka
Hivi ndivyo
vigeu utakavyotumia kutambua iwapo mada yake ina upe na mipaka maalum:
- Muda – iwe ya kutekelezwa kwa muda ufaao
- Gharama ya utafiti
- Vifaa utavyohitaji katika utafiti wako
- Faida ya utafiti. Je utapata maarifa mapya, tajriba
na jambo jipya litakalokujenga baada ya utafiti au la? Angalia manufaa
wala sio kufanya tu kwa ajili unahitajika kufanya utafiti.
- Ilete changamoto kwa mitazamo fulani ambayo jamii
imeshikilia. Kwa mfano, nafasi ya wanawake katika jamii.
- Ikuwezeshe na kurahisisha mbinu za kupata data yako
ili utekeleze kazi yako vyema. Kwa mfano, usichague mada ambayo unajua
hutapata data kwa urahisi. Mfano habari za jela, itakusumbua kupata kibali
kuwahoji wafungwa.
3) Maswali ya utafiti
i.
Mugenda na Mugenda (2012:281) wanasema
kwamba maswala ya utafiti yanapaswa kuwa:
(a)
Dhahiri
(b)
Bayana
(c)
Maalum
(d)
Mahususi
ii.
Haya ni maswahili mahsusi yanayoulizwa na
mtafiti kwa mujibu wa kauli ya uchunguzi ili kumsaidia na kumwelekeza katika
vipengele vya utafiti.
iii.
Huwa mafupi na bayana kwa kuwa yanatafuta
majibu yatakayoleta suluhisho katika suala la utafiti. (iv) Huweka mipaka kwa
kubainisha upeo wa utafiti na rasilmali zote kwa jumla.
iv.
Kila suala la utafiti huweka wazi aina ya data
inayonuiwa kukusanywa, na mbinu zinazohitajika kuifikia na kuichanganua.
Mfano
Mtafiti
anataka kuchunguza kiasi, kimo, upana au kina na sababu zinazohusu dhuluma za
kimapenzi miongoni mwa wafanyakazi wa sekta ya afya. Yafuatayo yatakuwa
miongoni mwa maswali yanayoweza kupelelezwa:
(a)
Dhuluma za kimapenzi zimeenea kwa kiasi gani miongoni mwa wafanyakazi wa kike?
(b)
Sera zipi kuhusu dhuluma za kimapenzi zinapatikana katika vituo vya afya?
(c)
Mafunzo katika masuala yanayohusiana na dhuluma za kimapenzi miongoni mwa
wafanyakazi yanatambuliwa kwa kiasi gani?
4) Malengo ya utafiti.
Malengo
ya utafiti hufafanua maswala maalum ambayo utafiti kutimiza.
Sifa
za malengo ya utafiti.
·
Huwa ni maelezo kamilifu ambayo
yanatarajiwa kutimizwa(SMART)
·
Yawe na uhusiano wa moja kwa moja na
swala la utafiti na yaweze kutafitika.
·
Yawe ya kuweza kutimika kwa wakati
mahsusi au maalum.
·
Hutoa muhtasari wa yale ambayo
yanakusudiwa kukamilishwa.
·
Huwa malengo maalum ambayo mtafiti
angependa kutimiza.
·
Huelekeza katika kupata majibu ya
utafiti lengwa kwa kuzingatia nadharia tete iliyopo.
Malengo
ya utafiti hugawika katika makundi mawili:
·
Malengo wazi/jumla
·
Malengo mahsusi
Malengowazi
na mahsusi si mamoja hivyo basi yasishughulikiwe kwa wakati mmoja.
Malengo
wazi.(General objectives)
·
Huwa mapana mno
·
Hueleza kile ambacho mtafiti angependa
kutafiti kwa kwa ujumla.
·
Huwa machache.
Malengo
mahsusi(Specific objectives).
·
Ni ya muda mfupi na yana upeo mdogo
sana.
·
Hupatikana tu baada ya kuvunjwa kwa
malengo wazi.
·
Hupatikana kwa kutimizwa kwa malengo
wazi
·
Huwa mengi mno
·
Ni lazima yaelekeze wazi mtafiti
atafanya nini, wapi na kwa nini?
Malengo
wazi hufafanua mchango wa utafiti katika uwanja mpana huku yakieleza bayana
lengo la utafiti.
Malengo
wazi ni malengo ambayo utafiti unakusudia kutimiza huku malengo mahsusi ni
matokeo hususan ambayo hujitokeza kwa wakati teule.
Umuhimu wa malengo ya
utafiti.
Malengo
ya utafiti:-
·
Humwezesha na kumwelekeza mtafiti kwa
kumpa mwelekeo ufaao wa kutafiti.
·
Humwezesha mtafiti kuepukana katika
kukusanya data data ambayo si muhimu katika utafiti husika.
·
Kupanga utafiti wake kwa utaratibu
ufaao.
·
Malengo mahususi yaliyopangwa ifaavyo
huelekeza utafiti kwa kuweka mbinu ambazo zinahakikisha kuwepo kwa Ukusanyaji, uainishaji na uchanganuzi wa data
ufaao.
Madhumuni ya
utafiti ni kutafuta majibu kuhusu maswali kupitia njia na taratibu za
kisayansi. Lengo kuu la utafiti ni kuvumbua ukweli ambao umejificha na haujavumbuliwa
na yeyote. Ingawa kila aina ya utafiti ina malengo mahsusi malengo ya utafiti
yanaweza kugawika katika makundi yafuatayo:
(i)
Kuelewa
swala fulani au kupata uelewa mpya. Tafiti kama hizi huitwa chunguzi (Exploratory or formulative research).
(ii)
Kudhihirisha
kwa usahili zaidi sifa za mtu fulani hali fulani au kikundi fulani. Tafiti hizi
huitwa tafiti elezi (descriptive).
(iii)
Kutathmini
kitu fulani hutokea mara ngapi baada ya muda fulani (frequency). Tafiti hizi
huitwa tafiti fumbuzi (diagnostic).
(iv)
Kutathmini
nadharia tete (haipothesia) ambayo inadhihirisha uhusiano wa kisababishi baina
ya vitu viwili. Tafiti hizi zinaitwa za tathmini ya ‘haipothesia’ (hypothesis – testing).
Marejeleo.
·
Adam, J na
Kamuzora, F (2008) Research Methods for Business and Social Studies. Morogoro:
Mzumbe Book Project.
·
Bowern, C
(2008) Linguistic Fieldwork: A Practical Guide. New York:
Palgrave- Macmillan.
·
Kothari, C.R
(2004) Research Methodology: Methods and Techniques. New Delhi: New
Age International.
·
Msokile, M
(1993) Misingi ya Uhakiki wa Fasihi. Nairobi: EAEP.
·
Mulokozi,
M.M. (1983) “Utafiti wa Fasihi Simulizi” katika TUKI Makala ya Semina ya
Kimataifa ya Waandishi wa Kiswahili III: Fasihi. Dar es Salaam: TUKI.: kur.
1-25.
·
Ogechi, N.O,
N.L Shitemi, na K. I. Simala (wah) (2008) Nadharia katika Taaluma ya
Kiswahili na Lugha za Kiafrika. Eldoret: Moi University Press.
·
Pons, Valdo
(Mh) (1992) Introduction to Social Research. Dar es Salaam: DUP.
·
Sewangi, S.S.
and Madumulla J.S. (eds) (2007) Makala ya Kongamano la Jubilei ya TUKI (Vol. I
and II) Dar es Salaam: TUKI.
·
Simala, K.I.
(mh) (2002) Utafiti wa Kiswahili. Eldoret: Moi University Press