Monday

utenzi wa Al inkishafi ' historia ilivyochangia kuibuka kwa kazi za fasihi

0 comments

 

KWA KUREJELEA UTENZI WA AL-INKISHAFI, ONYESHA NI VIPI HISTORIA HUCHANGIA KATIKA KUIBUA KAZI YA FASIHI.

Kwanza kabisa, ufafanuzi kwa kifupi  kuhusu dhana ya Historia na"uhakiki wa Kihistoria." Kulingana na Conkin na Stromberg (1989), Historia ni uchunguzi wa kweli kuhusu yaliyopita hasa kale ya binadamu. Hali kadhalika, kulingana na Kamusi ya Kiswahili sanifu (2004), uhakiki ni upataji wa hakika
au ukweli wa mambo. Maana ya pili ya uhakiki ni maelezo yanayochambua kazi ya fasihi kwa kuangalia mambo mbalimbali yaliyomo. Hivyo basi, uhakiki wa kihistoria ni lile tapo la uhakiki wa fasihi ambalo hujikita katika vyanzo vya kazi ya fasihi au matini ya fasihi kwa kujikita kwenye muktadha wa kihistoria wakati kazi hiyo ilipotungwa.

Kulingana na Keesey, uhakiki ambao unathaminiwa siku hizi ni uhakiki wa kihistoria. Anasema kuwa kazi yoyote ya fasihi inapaswa kuchunguzwa kwa kujikita kwenye muktadha wa mwandishi na muktadha wa utamaduni alimotungia mtunzi.

Kazi inafaa ichunguzwe kwa kurejelea mtunzi, maoni yake, itikadi yake, jamii yake, utamaduni, mambo yaliyopita na ya kisasa. Kila kipindi cha kihistoria huzalisha fasihi ambayo huakisi uhalisia wa kipindi hicho, wakati maalum na watu maalum. Kazi za awali zinaweza kuathiri matokeo ya kazi za sasa, na
kwa hivyo kuna umuhimu wa historia katika fasihi.

Kutokana na maelezo ya hapa awali basi uhakiki wa utenzi wa Al-inkishafi kihistoria unafuzu moja kwa moja.Utenzi wa Al-Inkishafi uliandikwa na mshairi Sayyid Abdalla bin Ali Nasir mzaliwa wa kisiwa cha Pate kinachopatikana kule Lamu. Huu ni baadhi ya tenzi kongwe ambazo zilitungwa katika miaka ya awali ama karne zilizopita.

Katika utenzi huu wa Al-Inkishafi, mtunzi ameangazia taswira halisi ya kihistoria ya wakazi wa kisiwa cha Pate. Haya yamejitokeza katika hali mbalimbali. Utenzj wa AI-Inkishafi umeshughulikiwa na wataalamu mba1imba1i. Utenzi huu u1ikusanywa na kutafsiriwa na Hichens(1972) katika A1-Inkishafi - The Soul's Awakening, ambapo pia umeshughu1ikiwa na J.V. Allen (1977) katika A1-Inkishafi -Catechism of a Soul. Halikadha1ika, utenzi huu umefasiriwa na  Muhamad wa Mlamali (1988) katika inkisiri ya Inkishafi.

Katika kazi yake, mashairi huyu mahiri anazama katika taswira kihistoria kwa kutujengea mazingira halisi ya Pate. Kisiwa hiki cha Pate kilikumbwa na mambo mbalimbali hadi kikaangamizwa. Kupitia katika utenzi huu upo uwezekano kuwa hali hii huenda ilimpa msukumo mashairi huyu.

Mshairi huyu amepewa sifa kedekede na Washairi pamoja na watafiti na wahakiki mbalimbali. Baadhi ya sifa anazopewa ni kama zifuatazo:

"Utenzi wa AI-Inkishafi wa Sayyid Abdalla A. Nasir ni mfano wa kazi ya kishairi ambayo zaidi ya kufaulu sana katika ujengaji wake wa taswira, ni kielelezo kizuri cha matumizi ya taswira za kiusambamba zinazotuchorea picha za  aina mbili kuu." Senkoro (1982:47)

"Al-Inkishafi ni utenzi usiokuwa na mwenziwe katika ushairi wa Kiswahili,utenzi ustahilio kuwekwa sambamba na baadhi ya tungo muhimu kabisa za mataifa mengin e y a u limwen gu ."Mulokozi (1971:58)

Mwandishi wa kifasihi huweza kuandika kazi yake kutokana na matukio Fulani ya historia. Tukio Fulani huweza kumwathiri mwandishi kiasi cha kumpa llhamu ya kuandika kuhusu tukio hilo au kuchota taswira zake kuzungukia tukio hilo kwa madhumuni ya kuuelimisha au kuutahadharisha umma.

Freeman Grenville (1975:241) anasema mengi kuhusu historia ya Pate, kwa mfano, aliyapokea kutoka kwa Bwana Kitini na masimulizi kuhusu historia hiyo yamehifadhiwa kwenye Tarikh ya Pate ( Pate Chronicles ). Baadhi ya matukio hayo pia yanaweza kupatikana katika kitabu cha C.H. Stigand (1966), The Land of the Zinj, mbali na matokeo ya utafiti wa historia chimbo.

Whiteley (1969:39) anasema kabla ya karne ya kumi kuna uwezekano kwamba Wabantu walitamalaki sehemu nyingi za ukanda wa Pwani. Halikadhalika, kulingana na Wana-historia kama MacCaster na Martin (1973), mji wa Pate haukuvumbuliwa na wageni hadi kufikia karne ya kumi na nne (1300), na kwamba mji huu haukufikia ufanisi hadi kwenye karne ya kumi na sita (1500).

Kulingana na Stigand (1966) pia tunafahamishwa kuhusu ushahidi wa .kihistoria hasa katika mambo ya kibiashara. Meli za mfalme Suleimani ziliwahi kufanya biashara na Ophir. Ijapokuwa hatuna ithibati ya kutosha kuweza kubainisha sehemu maalumu ilimokuwepo nchi hii, na hakuna ramani yoyote inayoonyesha-seheniu hiyo, baadhi ya watafiti wanadhania kuwa hii ni nchi ya Uhabeshi. Wengine wana mawazo kuwa ni Sofala ya zamani na kwamba ni yale machimbo ya mfalme Suleimani ya dhahabu ambapo meli zake zilibeba dhahabu mbali na pembe za ndavu na Tumbili. (Taz. Biblia)fmlango wa 10 kifungu 14-22). Hata hivyo, ufanisi wa mfalme Suleimani umekaririwa na Sayyid Abdalla katika AI-Inkishafi.

Ubeti 32.

Hakuwa mtume Suleimani

Maliki wa nasi na aJlnani

Walimufuteye ukamukhini

akiwa mwingine humtendaye?

Allen (1977:35)

Hili ni tukio la historia ambalo mbali na kwamba linatoa ithibati ya kuweko kwa mfalme huyo, linadhihirisha ukwasi aliokuwa nao hpta kumiliki binadamu na majini.

Ukoo unaosifika sana kisiwani Pate ni ule wa Nabahani. Ni ukoo wa kiarabu uliowahi kuitawala Oman kati ya 1154-1406 lakini baada ya kuanguka kwa ufalme huo, mfalme Suleimani alikimbilia Pate. Mbali na maelezo ya Freeman-Grenville(1975) kuhusu kustawishwa kwa usultani wa kinabahani Pate, Ahmed Sheikh Nabhany (kutokana na baadhi ya maandishi yake ) anasema  kwamba Suleimani alipokewa na Mfalme kutoka katika kabila la Oatawi. Suleiman aliozwa binti wa mfalme na baada ya fungate, akapewa zawadi ya ufalme wa Pate. Hivi ndivyo Nabahani walivyoanza kiutawala Pate.

Pate ikaanza kustawi kibiashara hata kuiteka miji jirani  kama vile Manda. Matokeo ya vita kati ya Pate na Manda yamesimuliwa katika ushairi wa Kiswahili ambapo Pate Iliibuka mshindi na kuwateka wenyeji wa Manda. Freeman-Grenville(1975:252) amedondoa ubeti ufuatao kuonyesha jinsi Wa-Manda waIivyonyanyaswa wakati mateka hao waume kwa wake, waIiIazimishwa kujenga ukuta mini Pate:

'Tuli kwetu Manda twali tukitenda

Yeo tukitendwa twakataa kwani?

Hutupa ukuta wathipetapeta

Kutwa ni kuteta, hatuna amani.

Kulingana na J.V. Allen (1977:17), Pate ilikuwa na ufanisi mkubwa na ikaweza kutawala mwambao wa Pwani hadi kufikia Kilifi karibu na Mombasa. Ufanisi huu ulitokana na biashara ya bahari ya Hindi, biashara ambayo ilimilikiwa na Pate wakati ambapo Kilwa, Mombasa, Malindi na miji mingine ya bara ilikuwa inatishwa na makabila kama vile Wagalla. Pia kulingana na J.S. Kirkman (1964:59), kuna uwezekano kuwa sehemu ya ufanisi huu ilitokana na uhusiano mzuri uliokuweko kati ya wenyeji wa Pate na Wagalla. Hawa waliweza kutoa mabawabu katika mji wa Patembali na bidhaa za ng'ombe kama vile ngozi. Mazao ya" mashambani, pembe za ndovu, kauri na magome ya kobe ni baadhi ya bidhaa zilizoiletea Pate ukwasi mkubwa wa kiuchumi. Kutoka Hindi, nguo za hariri zilipatikana ambazo zilibadilishwa na WaPate ili kupata shanga,chuma na nguo kutoka kwa Wareno.


Isitosh0, Freeman-Grenville (1975:255) anatueleza jinsi mpwa wa Sultani Omar alivyogundua kisiwa baharini kilichokuwa na madini ya fedha. Uvumbuzi huu uliiletea Pate ukwasi mkubwa kwani wenyeji wa Pate waliweza  kufua fedha hiyo na kujitengenezea mapambo mengi ya fedha. Ufuaji wa fedha ulichukuliwa kama sanaa muhimu kisiwani Pate.  Masonara walifua vyombo vya dhahabu, fedha na kwa sababu ya ufuaji huo wa fedha, Pate ilijulikana kama "Kiwang'aa" kwani mapambo hayo yaliiletea Pate sifa kubwa. Mapambo haya pia tunayakuta katika utenzi wa AI-Inkishafi, mapambo ambayo yalitumiwa na Wakwasi wa Pate kupambia majumba yao:

ubeti 37   Nyumba zao mbake zikinawiri

                   Kwa taa za kowa na za sufuri

                  Masiku yakele kama nahari

                 haiba na jaha iwazingiye

 

ubeti 38 Wapambiye sini ya Kuteua na

                kula kikombe kinakishiwa

               Kati watiziye kuzi na kowa

              katika mapambo yanawiriye.

              Allen (1977:37)

Beti hizi zinatuonyesha ukwasi uliokuwepo Pate. Hichens (1972:71) anasema kuweko kwa majumba yenye mng'ao yaliyonakshiwa vyombo vya Kichina na kauri kunamaanisha kwamba biashara kati ya Pate na Uchina ilikuweko. Ufanisi wa Pate pia ulitokana na juhudi za masultani wake kama vile sultani Mohammad bin Omar (Fumomadi) aliyestawisha kilimo na ujenzi wa vyombo vya kusafiria katika karne ya kumi na nne Casler na Martin (1973:25) nao wanasema kwamba Pate haikufikia ukwasi  wake hadi kwenye karne ya kumi na sita (1500). Sultani mwingine aliyechangia pakubwa katika ufanisi huo ni Swans mkuu bin Abubakr (1454-89) aliyepanua ustawi wa biashara. Kulingana na Freeman Grenville (1975:256) WaPate. Kuwepo kwa ufanisi huu ndiko kunakosimuliwa dhahiri katika AI-Inkishafi

Mbali na utawala wa Nabahani, wageni wengine waliowasili Pate, na ambapo pia wanagusiwa katika utenzi huu ni pamoja na Masharifu waliotoka Hadr8maut kutoka Yemen kusini. Masharifu hawa walikuwa katika makundi mbalimbali kama vile Sagaf, Shatiri (Sa Alawi) na Jamali lail (Jamal Al - Lail). Kulingana na E. Safi3, masharifu hawa walitoka sehemu za Shir na Tarim katika eneo la Hadramaut. Walifika mwambao wa Pwani kati yakarne za kumi na sita na kumi na nane. Kuja kwao kulitokana na sababu za kiuchumi, kisiasa na kijamii. Masharifu hawa wakiwemo watu wa ukoo wa Sayyid Abdalla waliwasili Pate. Pouwels (1987:40) kwa mfano, anasema wageni kutoka Senadir, Hadrami, na Yemen waliwasili mwambao wa Pwani na kwamba hawa walikuwa masharifu waliowasili sehemu za Lamu na Pate.

Baada ya majilio ya masharifu hawa, mitaa kama vile Sarambi, Inati na Shindoni iliibuka kwani wengi wao waliishi kwenye mitaa hiyo. Mtaa wa Inati kwa mfano, ulipewa jina hilo kutokana na masharifu waliotoka Inat ilhali ule wa Sarambi unaitwa hivyo kwa sababu Sarambi ulikuwa ukumbi uliojumuisha masultani, na Wasanii hasa hawa walipotongoa mashairi yao.



Mtaa huu pia uliishi Wanazuo na masharifu waliokuwa na ujuzi mwingi wa elimu ya dini kama anavyotuonyesha Sayyid Abdalla katika utenzi wake.

                       ubeti 59.          Wawapi wa kiungu wayaza kumbi

na masheke merna wake Sarambi?

Walaliye nyumba za vumbi vumbi

ziunda za miti ziwaaliye

Allen (1977:45)

Kuwepo kwa Wanazuo na makadhi mjini Pate pia kunasawiriwa katika AI-Inkishafi:

                 ubeti 62.    Kwali na maqadhi wamua haqi

Wahaqiqi zuo wakihaqiqi

Waongoza watu njema tariqi

Wasiwe kwa wote waitishiye.

Allen (1977:45)

Jambo lingine linalodhihirika katika utenzi huu ni kuhusu hali ya kiutawala iliyokuweko Pate. Watawala wa Pate walikuwa na nguvu za kiutawala na nguvu hizi zinadhihirika katika utenzi wa AI-Inktshafi ambao unasimulia ufanisi wa Patekatika kipindi cha historia ambacho bila shaka ni katika karne
ya kumi na nane.

Mambo haya yana ujumbe  muafaka kwani utenzi huu umesawiri mawaziri hao kwa uhalisi mkubwa:

            ubeti 36·         Wakimia mbinu na zaa shingo,

na nyuma na mbe1e ill miyongo,

Wakaapo pate ili zitengo,

askarl jamu wawatandiye

Hichens (1972:68)

Kwa upande mwingine, utenzi huu una uhusiano wa anguko la Pate.  Kufikia mwanzoni mwa karne ya kumi na tisa, Pate ilianza kuanguka. Mojawapo ya sababu za kuanguka ni vita vya wenyewe kwa wenyewe. J.V. Allen (1977:18) anatueleza kwamba mnamo mwaka wa 1820 AI-Inkishafi ilipoandikwa, ufanisi wa Pate ulikuwa umepotea.

Kulingana na maelezo ya baadhi ya Wana-historia hapo juu, ni dhahiri kwamba utenzi huu uliandikwa baada ya anguko la Pate. Mshairi Sayyid Abdalla bila shaka aliishi kuona nyumbani kwao kulikokuwa na ukwasi mkubwa kukiporomoka na kusalia magofu katika kipindi cha maisha yake.

Hichens (1972:37) kwa mfano, anaeleza kuwa utenzi wa AI-Inkishafi unapoelezea utamaduni na anguko la Pate, unatupatia mchango mkubwa kuhusu historia  ya Waswahili. Mmoja wa Malenga wa Mwambao huu aliulilia ufalme huo wa Pate ulioanguka.

Asili ya Pate-Yunga kuvundika

Mliondoka hadi na mpaka

Yea imekuwa pepe peperuka.

Hichens (1972:37)

 

Ghaidan (1975:13) anaona uhusiano uliopo kati ya utenzi wa AI-Inkishafi na matukio ya maanguko ya mji wa Pate anaposema:

 "AI-Inkishafi ni shairi lililoandikwa Pate katika mwongo huo ambapo linalilia siku zile za ufanisi."

Kumbukumbu za maanguko haya zinabainika katika beti kadha za utenzi huu. Katika beti hizi, mshairi anatolea kisa halisi na kutuonyesha yale yaliyosalia katika utawala huo.Anaposimulia kuhusu kimya kinachotawala kwenye magofu hayo na hata kutuonyesha baadhi ya wanyama na ndege waliofanya magofu hayo maskani yao, anatudhihirishia kwamba imebaki kusimulia tukio hilo. Uhalisi anaotuonyesha katika magofu hayo unatufanya tuhisi tukio hilo la kihistoria ambalo linapewa uhai wa kisanaa na mshairi.

 

 

                    ubeti 49.            Nyumba zao mbake ziwele tame;

makinda ya popo iyu wengeme.

Husikii hisi wala ukeme;

zitanda matandu walitandiye.

Hichens (1972:80)

 

                   ubeti 50               Madaka ya nyumba ya zisahani

sasa walaliye wana we nyuni

Bumu hukoroma kati nyumbani

zisiji na koti waikaliye

                   Ubeti 53:            Ziwanda za nyumba ziwele mwitu,

                                            ungi wa matuka na kutukutu,

                                            Milango ya ndia yatisha mtu,

                                           kwa kete na kiza kilifundiye

 

Katika beti hizi Sayyid Abdalla anayasawiri matukio ya kihistoria yaliyoufanya mji wa Pate kubaki magofu ambapo sasa wanyama mwitu ndio wametamalaki kwenye mahame hayo.

Tukizingatia matukio mbalimbali katika historia ya mwambao, tunaweza kufahamikiwa kwamba mwishoni mwa karne ya kumi na nane na mwanzoni mwa karne ya kumi na tisa, washairi walitunga mashairi ya upinzani dhidi ya utawala kutoka nje. Mfano mzuri wa washairi hawa ni kama vile Muyaka bin Haji (1770-1840). Lakini tokea mwanzoni mwa karne hiyo ya kumi na tisa, ushairi wa maombolezo unajitokiza zaidi. Huu ni ule uhalisi uliokuwepo katika maanguko na magofu ya nllji ya Pwani iliyokuwa na ufanisi mkubwa. Washairi walitunga tenzi zenyc usanii mkubwa kutoa maombolezo hayo. Kwa mfano, R. Oh1y (1977) katika makala yake, "The Bitter Attraction of the Bourgeoisie anatoa mfano wa shairi liitwalo 'Enzi nda Malhakatu', linalobainisha kuanguka kwa tabaka-tawala la Kimwinyi. Shairi hili linatoka sehemu za Lamu ambapo tabaka hili halikurithiwa na utawala wa nje bali kundi jipya lilirithi kutoka kwa tabaka la chini:

Walo wakitunga mbuzi na kukama na maziwa

Wakilimia minazi muini kutokuyuwa

Yea hutumia ezi kufunga na kufungua

Henda wakiyewayewa zitwa zili sakarani

( R.Ohly, 1977)

Ubeti huu unadhihirisha wazi sauti ya kuomboleza kutoka kwa mshairi, kuhusu kuanguka kwa tabaka tawala ambalo linaishilia kutawaliwa na wachungaji na wakulima.

Kw a hi v yom tun z i wa k is a r am b i c ha  Al - Ink ish a fi hakuachwa nyuma katika kuulilia wakati wa ufanisi wa Pate hasa anapojaribu ku1inganisha nyakati hizi mbili; wakati wa ufanisi na wakati wa maanguko, na hali ilivyokuwa.

Kutokana na hoja hizi, ni bayana kwamba utenzi wa AI-Inkishafi unatusimulia habari halisi za matukio ya kihistoria. Utenzi unatupa hifadhi ya kudumu kuhusu ufanisi na maanquko ya Himaya ya Pate. Kupitia kwa beti zake, tunaweza kuhisi, sauti ya maombolezo kuhusu ukwasi wa mji wa Pate ambao sasa umesalia kijiji tu cha vibanda vya matope.

Jambo lingine ni kwamba Sayyid Abdalla aliishi kuona ukwasi wa Pate na pia kushuhudia anguko lake (Allen 1977:18). Kwa hivyo, utenzi huu ni kielelezo halisi cha falsafa yake binafsi ambayo aliiteua kulingana na tajriba yake. Hapa tunaona jinsi msanii anavyotumia tukio la historia kuendeleza dhamira ya kazi yake. Halikadhalika, kazi ya msanii wetu imejikita kwenye nadharia yetu kwani tunaona jinsi anavyotumia matukio ya historia katika mazingira yake na kulingana na wakati wake kututolea dhamira yake.

Kwa hivyo, mbali  na kule kushuhudia matukio hayo, Sayyid Abdalla aliishi kuwaona Wakwasi hao anaowasawiri wakiogelea katika utajiri wao. Aliishi kuwaona Makadhi waliosheheni elimu ya dini pamoja na wale mamwinyi waliomiliki nyenzo za uzalishaji mali. Bila shaka alifahamu maisha ya watu hao na maishilio yao ya k uweza k u s im ulia k am a alivyo fan ya katika utenzi wa Al-Inkishafi.

Kwa upande mwingine, inadhihirika kuwa mashairi huyu ametumia taswira ya kimazingira ya Pate katika utenzi wake.Mazingira haya yanaweza kuwa ya kijiografia,kijamii, kiuchumi na kiisiasa .

Katika mfumo wa kijiografia, Kisiwa cha Pate kimezungukwa na bahari ya Hindi na kimetengwa na bara na mlangobahari wenye uhaba wa maji na ambao Kulingana na Brown Howard (1985:14), una upana wa maili moja. Kisiwa hiki pia kimezungukwa na mikoko ambayo imesababisha ugumu katika usafiri wa maji kwani huzuia vile vijia na ghuba ndogo za kuingilia kisiwani. Kwa hivyo ni dhahiri kwamba Sayyid Abdalla alitumia kikamilifu mandhari haya ya pwani kwa mfano, anapotongoa ubeti wa 13 katika AI-Inkishafi.

                                      ubeti 13         Suu ulimwengu bahari tesi

una matumbawe na mangi masi

Aurakibuo juwa ni mwasi

Kwa  kulia khasara ukhasiriye

(Mlamali 198O:17)

Mtunzi aliishi kuiona shwari na michafuko ya bahari pamoja na matumbawe yaliyomo ndani yake ambayo yangeweza kukwamisha chombo. Anatumia ujuzi wake wa bahari katika kutuonyesha picha  ya u1imwengu kama tutakavyoona baadaye.

Halikadhalika, kisiwa cha Pate hupata aina mbili za majira ya mvuaj mvua za kusi (masika) ambazo hutokea upande wa Shanga iliyo kusini mwa Pate, na mvua za kaskazi ambapo upepo unaotoka kaskazi huleta majahazi kutoka Manga na Bara Hindi. Habari hizi zinathibitika kwani Howard (1985:14) pia anasema misimu ya mvua ni mbili kwa mwaka. Kuna mvua za mwaka ambazo huwa, ni kati ya Aprili hadi Juni, na mvua za vuli kati ya Julai na Novemba. Mvua katika sehemu hii ni chache mno na aghalabu haiwezi kutegemewa. Hii ndio sababu wenyeji wa Pate walithamini sana maji ya visima.

 Kila nyumba  ilikuwa na kisima na kuna vile vilivyokuwa nje ya mji ambavyo ndivyo visivyokuwa na Ombe. Mara nyingi visima vya aina hii vilipatikana katika vitangu nje ya mji Naye J.V. Allen (1977:76) anasema aina hii ya visima ilipatikana nje ya mji mahali ambapo watu wa tabaka la chini walinywesha mifugo yao na hawakuwa na uwezo wa kuchimba visima katika nyumba zao. Visima hivi havikuwa na kina kirefu kama anavyotongoa Sayyid Abdalla:

 

 

                         ubeti 14           Ni kama kisima kisicho ombe

Chenye mta-paa mwana wa ng'ombe

Endao kwegema humta pembe

asipate katu kunywa maiye

(Allen 1977:29)

Kisiwa cha Pate ni tambarare na kwa ujumla ni ardhi kame iliyo na vichaka hapa na palepamoja na wingi wa mikoko ambayo imechukua sehemu kubwa ya eneo la Pate. Hali hii huzuia kilimo cha mapana. Udongo ni wa changarawe usio na rutuba lakini sehemu zingine zina udongo mwekundu ulio na rutuba kiasi. Hapa na pale kuna matumbawe yaliyojitokeza kwenye ardhi. Kwa sababu ya uchache wa mvua, hali ya anga huweza kuwa na jua kali mno hasa wakati wa adhuhuri kwenye jua la utosi. Ukali wa jua huweza kusababisha maziqazi hasa katika sehemu tambarare kama hizi. Halikadhalika. katika majira ya kiangazi  kama anavyokiri Mlamali (1980: 19 ), sehemu  za pwani huwa na jua kali na ardhi kavu. Hali hii hususan vumbi jingi angani na jua linapochomoza saa za alfajiri hulikumba lile vumbi likaonekana kama kitu ambacho chaweza kushikika. Hali hii anaieleza mshairi wetu ambaye bila shaka ni kutokana na uhalisi wa vitu hivi alivyoviona:

                             ubeti 15     Au enga vumbi la muangaza

Wakati wa yua likitepuza

Mwenda kulegema akilisaza

asiane kitu ukishishiye

 

                           ubeti 16       Au enga meta 1imetukapa

Wakati wa yua lilinganapa

Mwenye nyata hwamba 'ni mai yapa'

Kayakimbilia akayatwaye.

( Mlamali 1980:19).

Kwa hivya vumbi la mwangaza na mazigazi mtu anayaona wakati wa jua kali ni vieleleza ambavyo mshairi anavitumia kutakana na mazingira halisi ya Pate. Kabla ya mwanza wa msimu wa mvua Wapate walitia vichaka mota ili kujitayarisha kupanda mbegu. Hii ni desturi iliyakuweka hasa katika sehemu ya bara iliyapakana na kisiwa.


Aghalabu mvua ya radi iliweza kutakea ghafla bila matarajio ya watu waliakuwa k~tika harakati za kutayarisha mashamba yaa. Mvua hii ilitatiza juhudi za matayarisha kwani ni vigumu mota kuwaka katika kichaka ki1ichakalea maji ya mvua. Haya ndiyo ayaanayo mtunzi wa Al-Inkishafi:

                            ubeti 29.      Au enga mota kururumika

Ulio weuni katika tuka

Pakashuka wingu katika chaka

ikawa kuzima usiviviye.

(Hichens 1939:64)

Kwa hivya katika beti tu1izodandoa hapo juu, ilidhahirisha kwamba mshairi alitumia uhalisia wa kimalisha katika mazingira yake ili kufikia dhamira yake.

Kwa kutazama mrengo wa kijamii, hasa kulingana na Knappert (1967:39), ni kwamba Waswahili halisi waliitwa Waungwana yani watu huru ilhali wale wa tabaka la chini walijulikana kama Watwana. Howard (1985) naye asema jamii hii ni kusanyiko la watu wenye tamaduni mbalimbali katika mazingira ya miji. Tabaka mbalimbali zilizuka kutokana na aila za watu hao na ziliishi  katika mitaa maalum. Howard anaainisha tabaka tatu maalumu tabaka la Waungwana ambalo lilijumuisha watu hu:ru, tabaka la wazalia yaani wale waliozaliwa na watumwa katika majumba ya matajiri, na tabaka la chini ambalo Iilijumuisha watumwa ambao pamojana Wazalia walifanya kazi ya kuwatumikia mabwana matajiri. Kwa kulitomelea wazo hili, Mulokozi (1975) naye anasema wengi wa Washairi walitoka katika tabaka la juu kwani ndio waliokuwa na njia za kujiingiza katika utajiri huo.

Kutokana na mawazo haya, ni dhahiri kuwa jamii ya Waswahili katika siku za Sayyid Abdalla, ilikuwa ya kitabaka. Tabaka la Waungwana lilikuwa tabaka tawala. Tabaka hili lilijumuisha koo zilizostawi katika mji na ambazo zilimiliki nguvu za kisiasa --A-akiuchumi. Lilikuwa na jukumu la kustawisha viwango vya utamaduni na lilihusisha wataalamu wa elimu ya dini, watu walioishi katika majumbe  ya' mawe na waliokuwa na mashamba nje ya mji ndio walioshiriki katika biashara kubwa kubwa za ulanguzi, kumiliki zana za uzalishaji mali pamoja na mambo ya kisiasa. Waliamini kuwa nyadhifa hizi ni kulingana na majukumu yaliyoanzishwa na mababu zao hasa katika uanzilishi wa miji ya pwani.

Kwa hivyo ni dhahiri kwamba Sayyid Abdalla alipotunga AI-Inkishafi, aliielewa jamii iliyomzunguka hata kujimudu kuisawiri kikamilifu. Kuhusu tabaka hili la Kimwinyi, mshairi alitongoa hivi:

                   ubeti 34     Uwene wangapi watu wakwasi

  Walo wakiwaa kama Shamsi

 Wamuluku zana za adharusi

 dhahabu na fedha wakhiziniye

Kwamba ukwasi wa watu hawa uliwafanya wamiliki zana za vita, ni jambo lililakuwa si kawaida kwa Pate ya karne ya kumi na tisa.

                Ubeti 35      Malimwengu yate yawatiile

Na dunia yao iwaokele

Wachenda zitwa zaa zilele

Mata mafumbuzi wayafumbiye

 

            ubeti 36         Wakimia mbinu na zao Shingo

na nyuma na mbele ili miyongo

Wakaapo pote ili zitengo

askari jamu wawatandiye.

(Allen 1977:37)

Katika beti hizi kinadhihirika kiburi cha matajiri hao pamaja na heba na jamali waliyokuwa nayo. IsItoshe, kule kuweko na mistari ya walinzi na pia kule kutengewa mahala pao maalum pa kukaa ni dhihirisha la uhalisi katika maisha ya anasa ya watu hao. Kwamba malimwengu yote yaliwatii ni dhihirisho kuwa waliishi kutegemea jasho la wengine . Dhana ya ut umishi au utumwa inadhihirika katika ubeti huu:

 

                    Ubeti 40                       Kumbi za msana ili kuvuma

na za masturi zikiterema

Kwa kele za waja na za khudama

fwraha na nyemi zishitadiye

(Allen 1977:37)

Sura nyingine ya kijamii ambaya inajitakeza katika utunzi wa AI-Inkishafi ni kule kuweka kwa mitaa. Mtaa ulichukuliwa kama taasisi iliyawakubali wakimbizi kutangamana na wenyeji .Ki1a mji, hata mji wa Pate, u1ikuwa na mitaa. Howard (1985:49) kwa mfano, anasema kulikuweka na mikao yaani sehemu za mji zi1izogawanyika katika pande mbili na hizi zilistawishwa na waungwana. Katika mikao hii kulikuwa na mivutana ya kijamii lakini Haward anasema migangana hiya pia llisababisha kustawi kwa mji kiutamaduni, hasa kisanaa. Kwa mfano, ni kupitia kwa mashindano ya ngoma  na ushairi ambapo  mikao hii i iliweza kukumbana na hivyo kuleta muungano thabiti. Sayyid Abdalla anatongoa haya kuhusu mitaa hiyo:-

                 ubeti 59     Wapi wa Kiungu wayaza kumbi

na Mashekhe mema ya Ki-sarambi

Walaliye nyumba za vumbi vumbi

Ziunda za miti ziwaaliye.

Sarambini ni mtaa ambapo Masharifu, ikiwemo jamaa ya Sayyid Abdalla, waliishi pamoja na Mashekhe na viongozi wengine. Ni hapa pia ambapo Washairi walitongaa mashairi yao na Mashekhe walijaza kumbi za mazungumzo kuhusu mambo mbalimbali. Maisha ya Kimwinyi katika majumba ya matajiri yamesawiriwa katika beti zifuatazo:

 

 

              ubeti 49         Nyumba zao mbake ziwe1e tame.

makinda ya papa iyu wengeme.

Husikii hisi wala ukeme

Zitanda matandu walitandiye.

 

             ubeti 50         Madaka ya nyumba ya zisahani

Sasa wa1a1iye wana wa nyuni

Bumu hukoroma kati nyumbani

Zisiji na koti waikaliye

(M1ama1i 1980:47-48)

Nyumba zao zi1ing'ara kwa mapamba ali ali yaliyohifadhiwa kwenye madaka. Nyumba anazae1eza mshairi ni zi1e za miraba minne na ambazo zilikuwa na rafu zilizojengewa kwenye nyumba hizo ili kuweka vyombo vya kaure na mapambo mengine. Nyumba hizi kwa kawaida zi1ikuwa na vyumba viwili au vitatu virefu; kuna msana wa tini, msana wa yuu na sehemu ya ndani ambayo aghalabu i1itengewa wanawake. Kwa hivyo kumbi katika misana hii kama anavyosema mshairi ilikwishamilikiwa na ng’ende kama vile vidaka ambavyo vilikuwa makao ya nyuni.

               ubeti 52         Nyumba kati zao huvuma mende

Kumbi za msana hulia ng'ende

Yalifiye vumi makumbi ya nde

Kuwa mazibala yalisiriye

(Mlamali 1980:49)

Bila  shaka Sayyid Abdalla alizuru magofu ya mji wa Pate kabla ya kujiandaa kuandika Inkishafi kwani mazingira halisi anayotupitisha katika mahame hayo ni kielelezo kamili cha maisha ya anasa yaliyotoweka. Mshairi huyu bila shaka aliishi maisha hayo kwani anavyotudondolea matandiko ya wakwasi hao, namna ya kula kwao na vyombo wanavyotumia ni baadhi ya vielelezo vya maisha ya Kimwinyi:

             ubeti 42        Kwa maao mema ya kukhitari

Iyu la zitanda kwa majodori

Na mito kuwili ya akhadhari

na kazi ya pote wanakishiye

(Mlamali 1980:41)

 

 

           ubeti 38            Wapambiye sini ya kuteua

na kula kikombe kunakishiwa

Kati watiziye kuzi za kowa

Katika mapambe yanawiriye

(Mlamali 1980:40)

Kwenye upande wa kidini, ni Kwamba kwa kiasi kikubwa Sayyid Abdalla alitumia mazingira na tajriba yake ya dini katika sanaa yake na ni jambo linaloweza kutolewa ithibati. Mwandishi huyu alikuwa mfuasi kamili wa dini ya kiislamu na kuna vipengele vya kuthibitisha haya. "Bismillah" ni tamko muhimu katika Uislamu na kwa mujibu  wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu (1981), neno hili husemwa kabla ya kufanya jambo lolote jema. Neno hili huwa na maana ya "Kwa jina La Mwenyezi Mungu". Ni neno la kwanza katika ubeti wa kwanza wa nudhumu hiyo ya Inkishafi.

                      ubeti 1              Bismillahi naikadimu

hali ya kutunga hino nudhumu

Na ar-Rahmani kiirasimu

basi ar-Rahimi nyuma ikaye.

(Mlamali 1980;1)

Matumizi ya maneno ar-Rahmani na ar-Rahimi humaanisha Mungumwenye rehema na mwenye kurehemu. Haya kutokana na muktadha huu hutamkwa muislamu anapoanza kazi yoyote mpya na aghalabu hutumika mwanzoni mwa kazi ya uandishi. Amali za Uislamu pia zimejitokeza katika ubeti wa nne wa Inkishafi. Anataja sahaba wanne yaani wale makhalifa wa mtume Muhamadi. Kwa kuwataja haw a wanne pekee miongoni mwa wengi, kunaweza kutuashiria' kuwa mtunzi W8 Inkishafi alikuwa Mwislamu wa madhehebu ya Sunni madhehebu ya Shia , kwa mfano angemtaja sahibu mmoja tu  Ali:

                ubeti 4             Naalize thamma, Banu klnana

     na sahaba wane wenye maina

    Tusalie wote ajmaina

    sala na mbawazi ziwaaliye.

     (Mlamali 1980:5)

Kulingana na J.V Allen (1977:77), Sayyid Abdalla alikusudia hawa kuwa makhalifa wanne; Abu Bakr, Umar, Uthman na Ali. Katika ubeti wa tatu wa Inkishafi tunakutana na neno "Tumwa" ambalo linaanza na herufi kubwa:

            ubeti 3            Ikisa himdi kutabalaji

ikituzagaa kama siraji

Sala na salamu kiidariji

Tumwa Muhamadi tumsaliye

(Mlamali 1980:5)

Neno hili lina maana ya "Mtume" na katika utenzi huu limetumiwa kumtaja mtume mmoja tu, yaani mtume Muhamadi. Kutajwa kwa Muhamadi kunasisitiza tu umuhimu wa mtume Muhamadi.

Jambo lingine ambalo hatuna budi kulichunguza ni juu ya Wasomi wa dini ya kiislamu. Tabaka la Kimwinyi lilijumuisha pia masharifu na makadhi waliokuwa weledi sana wa falsafa ya kiislamu. Kulikuwa na waandishi na wafasiri wa tenzi zilizoandikwa katika kipindi alichoishi Sayyid Abdalla. Hakuna mwandishi au mshairi anayeweza kulaumiwa kwa mfano, kwa kutumia maudhui na taswira za kidini. Kwa hivyo, dini ni kigezo muhimu kilichotumiwa kustawisha mfumo wa Kimwinyi uliokuwepo.

Knappert (1967) pia anatueleza kuwa waungwana hawa waliutumia muda wao mwingi katika misikiti wakisoma na kufasiri vitabu vitakatifu na kushiriki katika mijadala ya kidini. Mtunzi wa AI-Inkishafi anawasawiri mamwinyi hao katika ubeti huu:

                 Ubetu 62    Kwalina makadhi wamuwa haki

 Wahakiki zuo wakihakiki

Waongoza watu njema tariki

Wasewe kwa wote waitishiye.

(Mlamali 1980:55)

Kwa hivyo ni dhahiri kuwa Sayyid Abdalla mbali na kuwa mshiriki wa dini ya kiislamu, aliyafahamu majukumu ya makadhi na wahakiki wa maandishi ya kidini na kuweza kubainisha kuweko kwa watu hao katika jamii yake.

Vile vile historia ya kiuchumi ya wakazi wa Pate pia  imejitokeza wazi katika utenzi huu. Kisiwa cha Pate mbali na kujihusisha na biashara ya utumwa, kilijihusisha pia na biashara ya kimataifa na huenda biashara hii ndiyo iliyosababisha kuimarika na kustawi kwa mji wa Pate.Biashara ilistawi kutokana na teknolojia muafaka ya bahari na ufahamu wa kutosha kuhusu pepo na mikondo ya bahari ya Hindi. Pepo za bahari zilivu ma kulingana na misimu; pepo za kaskazi-mashariki zilianza kuvuma tokea Novemba hadi Machi na zile za kusini-magharibi zilivuma tokea Juni hadi Septemba. Pepo hizi zilisaidia vyombo vya bahari kusafiri kutoka sehemu kama Ghuba la Uajemi na bara Hindi hadi mwambao wa Afrika Mashariki. Menyeji wa Pate hasa wale matajiri walichukua nafasi ya kati katika biashara hiyo. Walipokea bidhaa kutoka bara kama vile pembe za ndovu, ngozi, magome ya kobe, na zile nguzo za mikoko ambazo zilitumiwa  kuzibadilisha na bidhaa za kutoka ng’ambo.

 

Bidhaa  zilizotokanchi za nje zilikuwa ni pamoja na  vyombo vya sini, hariri, ngano, pamba na bidhaa zinginezo. Wageni kama vile Waarabu, Waajemi, Wahindi na Wareno ni baadhi ya wale waliofanya biashara na Pate. Kwa mfano, Strandes (1961:151) anasema Pate ilitegemea sana vitambaa vya nguo na mchele kutoka bara Hindi.na shanga kutoka Uchina. Wareno walileta mvinyo, matumbawe na Unga. Pate pia ilipokea dhahabu kutoka katika sehemu zilizopakana na Kilwa.

Pate ilisifika sana kwa uzalishaji wa vitambaa vya kufumwa vyenye rangi za kuvutia. Ufuaji wa vyombo vya shaba na fedha ni sanaa iliyosifika pia Pate kwani wana sanaa walizalisha vyombo tofauti vya dhahabu1 fedha na mapambo ya thamani. Kwa hivyo ni dhahiri kusema kuwa biashara kutoka nje iliwaletea Wapate vifaa vya kujipambia tu bali sio bidhaa za kuzalisha mali. Basil Davidson (1969:167) analalamikia hali hii akisema kwa muda "mrefu Afrika ya Mashariki ilikuwa chemchemi kuu ya dhahabu zilizochotwa na kuhamishwa Asia na Uarabuni. Sayyid Abdalla anayasawiri mapambo hayo katika utunzi wake hivi:

               Ubeti 34                   Uwene wangapi watu wakwasi

walo wakiwaa kama shamsi

Wamuluku zana za adhurusi

dhahabu na fedha wakhiziniye

(Mlamali 1980:38)

Kwa sababu ya wingi wa fedha na dhahabu tabaka tawala la Kimwinyi ambalo ndil0 lililomiliki biashara hiyo, lilifaidi kutengeneza mapambo yaliyonakshiwa fedha na dhahabu. Halikadhalika, mapambo kama vile kowa na sufuri yaliyoagizwa kutoka bara Hindi yalitumiwa namatajiri hao kunakshia taa zao kama mshairi wa Al Inkishafi anavyobainisna:

                      Ubeti 37    Nyumba zao mbake zikinawiri

                                           kwa taa za kowa na za sufuri

                                           Masiku yakele kama nahari

                                           haiba na jaha iwazingiye

(Mlamali 1980:39).

Katika karne za kumi na saba na kumi na nane, Pate ilifikia kilele cha ufanisi. Vyombo vya sini vikiwemo makuzi na makowa viliagizwa kwa wingi kutoka Uchina na wingi wa mapambo haya uliashiria utajiri wa Wakwasi hao:



 

 

                     Ubeti 38   Wapambiye sini ya kuteuwa

na kula kikombe kunakishiwa

Kati watiziye kuzi na kowa

Katika mapambe yanawiriye

(Mlamali 1980:40)

Ule umaarufu wa kufuma vitambaa vyenye rangi za kupendeza ambavyo aghalabu vilipewa wana wa wafalme na matajiri kama zawadi (Strandes 1961:78-79) pia unasawiriwa na mshairi ili kudhihirisha ustawi wa biashara ya nguo za hariri na sanaa ya ushonaji:

           Ubeti 42           Kwa maao mema ya kukhitari

iyu la zitanda kwa majodori

Na mito kuwili ya akhadhari

na kazi za pate wanakishiye

(Mlamali 1980:41)

            Ubeti 43          Misutu mipinde wakipindiwa

iyu la firasha kufunikiwa

Mai ya marashi wakiukiwa

itiri na kaa waipashiye

( Mlamali 1980:42)

Sanaa ya upote pamoja na utengenezaji wa mito kwa mfano, ni shughuli ambazo  huenda zilifanywa na Wapate wenyewe. Strandes (1961:89) kwa mfano, anasema kuhusu sanaa ya ushonaji kwamba Wareno waliowasili Pate katika karne za kumi na sita na kumi na sabat walieleza juu ya hariri bora na nguo zilizofumwa kwa ujuzi mjini Pate. Naye Howard (1985:167) anaonyesha kuwa kulikuwa na mpamba mwitu, aina ya pamba iliyojiotea ovyo msituni katika sehemu nyingi za pwani. Pamba hii huenda ndiyo iliyotumiwa pamoja na ile iliyoagizwa kutoka bar a Hindi, kuzalisha bidhaa za nguo. Msufi mwitu ni aina nyingine ya sufi iliyotumiwa kwa mfano, kutengenezea mito. Strandes anaendelea kusema koo za an-Nadir pamoja na Jamali lail zilijulikana sana katika utengenezaji wa kanzu na vikoi.


Bidhaa kama marashi pia yaliagizwa kutoka nje ilhali kaa ni aina ya mti uliosagwa na kutengenezwa manukato. Wanawake walifanya kazi hii katika kujirembesha. Itiri pia ni aina ya manukato iliyoagizwa kutoka nje. Bidhaa nyingine zilizotoka nje ni kama misaji na abunusi, alna za mbao zilizotoka bar a Hindi. Mbao hizi zilitumiwa kutengenezea changoza kutundikia nguo na mapambo mengine. Sayyid Abdalla anatuhakikishia kwamba aina hizi za mbao za thamani kubwa, ziliweza pia kumilikiwa na matajirikutokana na ule umilikaji wa biashara hiyo.


          Ubeti
39               Zango za mapambo kwa taanusi

naapa kwa Mungu Mola Mkwasi

Zali za msaji na abunusi

Zi tele sufufu zisitawiye

(Allen 1977:37).

Mbali na biashara, Pate ilijishughulisha na kilimo ambapo matajiri wa  Pate walimiliki mashamba barani ambayo yaIinadhifiwa na watumwa Uvuvi pia ni shughuli nyingine iliyoendelezwa Pate pamoja na  ujenzi wa mitepe na mashua za usafiri wa maji. Maisha ya kisiasa pia yamejitokeza wazi katika utenzi huu. Kiserikali, Pate ilikuwa na Sultani  ambaye alisaidiwa na kupewa ushauri na watu wakuu kama mawaziri. Lakini baadhi ya viongozi hao aghalabu walikabiliwa na upinzani kutoka kwa washauri na watukufu wengine wa mji. Lakini pia tunaweza kusema uongozi huu pia ulikabiliwa na matatizo kwa sababu hakukuwa na kanuni au sheria maalum za kufuatwa hasa katika mirathi ya kifalme. Huenda jambo hili liliwafanya baadhi ya viongozi hao kujiwekea vikosi vya askari ili kuimarisha usalama wao. Hivi ndivyo ilivyokuwa katika wakati wa mtunzi wa AI-Inkishafi kwani anatuonyesha jinsi watawala hao walivyotengewa mahali pao maalum pa kukaa, najinsi walivyolindwa na makundi ya askari:

             

 

               Ubeti 36        Wakimia mbinu na zao shingo

na nyuma na mbele ili miyongo

Wakaapo pote ili zitengo

askari jamu wawatandiye

(Allen 1977:37)

            Ubeti 61          Kwali na mabwana na mawaziri

Wenda na makundi ya Askari

Watamiwe na nti za maqaburi

Pingu za mauti ziwafundiye.

(Allen 1977:45).


Dini ya kiislamu ilitumiwa kama kigezo muhimu katika kustawisha mfumo wa kisiasa nyakati za umwinyi. Kwa mfano, wenyeji walitakiwa wamtii sultani au mfalme pamoja na Mungu. Sura hii inaonekana katika utendi wa Al- Inkishafi.

                 Ubeti 35      Malimwengu yote yawatiile

na dunia yaa iwaokele

Wachenda zitwa zaa zilele

Mata mafumbuzi wayafumbiye

(Allen 1977:37)

Katika sehemu hii imedhihirika  kwamba kwa kiasi kikubwa, mazingira alimoishi Sayyid Abdalla yana uhusiano wa moja kwa moja na sanaa yake. Tajriba yake katika maisha ya kijamii ya Pate, hali za kiuchumi zilizakuweko pamoja na taasisi zinginezo zilichangia kiasi kikubwa katika kueleza dhamira yake. Dini yake ya Kiislamu pamoja na amali zilizoko katika djini hii pia vinlechangia pakubwa katika kukamilishe maudhui ya kazi yake.

 

Hitimisho

Utenzi wa In-nkishafi umetanda na kutawala kihistoria kuhusu kisiwa cha Pate kipatikanacho Lamu. Utenzi huu umezama katika vitengo mbalimbali vya maisha ya wakazi wa eneo hilo. Hii ni pamoja na amali zao, mila, miiko, siaisa, biashara bila kusahaulia mbali utangamano uliotanda katika kisiwa hicho kati ya wakazi hao na jamii za kimataifa ambazo zilikiona kuwa mojawapo wa visiwa maarufu mwambaoni.

Utenzi huu vile vile umeweka wazi mihimili iliyokiweka imara kisiwa hiki pamoja na kuporomoka kwacho. Umeangazia baadhi ya sababu ambazo zilikiporomosha kisiwa hicho. Kisiasa katika kisiwa hicho, utenzi huu haukusahaulia mbali bali ulibainisha wazi namna viongozi walivyokuwa wakiingia uongozini pamoja na majukumu yao teule.

Kwa kuwa dini ya kiislamu imetanda katika mwambao, jamii hii imelivalia njuga swala hili. Utenzi huu katika utangulizi wake kwenye ubet wa kwanza, umedhihirisha wazi kuwa ni jamii ambayo inamcha Mungu kutokana na namna inavyoheshimu swala zima la kidini.

Marejeleo.

a.       Dawood, N.J. ( Translator) (1974) The Koran. Harmondsworth: Penguin Books De Vere Allen (1977) Al Inkishafi: Catechism of the Soul. Nairobi: East African Literature Bureau

b.      Hitchens, W. Al-Inkisafi: The Soul’s Awakening. Nairobi: Oxford University Press,

 

c.       Kiptanui,G. D. R. (19980 Uhusiano wa Sitiari na Tashbihi na Mazingara ya Mwandishi. Unpublished M. A. Thesis, University of Nairobi

 

d.      Mulokozi, m. M. (1999) Dar es Salaam: Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili

e.       Wa Mberia (1986) Maudhui Katika Al-Inkishafi”. Unpublished seminar paper, University of Nairobi

 

f.       Wa Mlamali, M. (1980) Inkishafi: Ikisiri ya Muhamadi wa Mlamali. Nairobi: Longman

g.       Wafula, R.M. (1992). "Nadharia kama mwongozo wa utunzi na uhakiki katika
fasih!". Makala ya Semina. (Hayajachapishwa)

h.      Nyerere, J.K. (1973). Ujamaa ni imani: Moyo kab/a ya silaha. Dar es
Salaam:East African Publishing House.

i.        Nyanchama, M.B. (2004). "Matumizi ya Taswira na Ishara katika Sauti ya
Dhiki." Tasnifu ya M.A. Chuo Kikuu cha Kenyatta. Nairobi
(Haijachapishwa).

j.        Msokile, M. (1993). M(singi ya Uhakiki wa Fasihi. Nairobi: East African
Educational Publishers Ltd.

k.      Momanyi, C. (1991) "Taswira kama Kielelezo cha Uhalisi katika Ujenzi wa AIInkishafi" Tasnifu ya M.A. Chuo Kikuu cha Kenyatta, Nairobi
(Haijachapishwa).

l.        Mbunda, M. (1993). Misingi ya Uhakiki wa Fasihi. Nairobi: East African
Educational Publishers Limited.

m.    Gakuo, J. K. (2010). "Ufasiri na Uhakiki wa Kihemenitiki wa Ushairi wa Kiswahili". Tasnifu ya
Uzamifu, Chuo Kikuu cha Kenyatta. Nairobi: Kenyatta (Haijachapishwa).

n.      Wamitila, K. W. (2003). Kamusi ya Fasihi: Istilahi na Nadharia. Nairobi: Focus Books.

 

 

 

No comments:

Post a Comment